Header Ads Widget

CHAMA CHA MAPINDUZI MKOANI IRINGA KIMEMPONGEZA RAIS Dkt. SAMIA

 

Chama cha mapinduzi (CCM)mkoa wa Iringa, Kimempongeza  Rais wa Tanzania DR. Samia Suluhu Hassan kwa kuruhusu kufanyika kwa mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa .


 Kuwa jambo hilo ni muendelezo wa ukuaji wa demokrasia hapa nchini.


Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) mkoa wa Iringa Daudi Yassin, wakati akizungumza na wanahabari mkoani hapa leo Ijumaa Januari 6,2023, na kuongeza kuwa ruksa ya kuanza kwa mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa hapa nchini, isiwe chanzo cha vurugu wala uvunjifu wa amani miongoni mwa watanzania.


Mwenyekiti huyo amesema baada ya ruhusa ya mikutano chama cha mapinduzi mkoa wa Iringa kimejipanga vyema kuanza mikutano ya hadhara bila hofu wala uoga kama inavyosemwa na baadhi ya ya wapinzani.


Katika hatua nyingine amevitaka vyama vingine kuitumia vizuri fursa hiyo kwa kufanya mikutano yenye tija, kwa kuzitangaza sera na mipango ya vyama vyao kwani wao watakwenda kuwatangazia wananchi juu ya utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi ambayo ndiyo inaongoza nchi kwa sasa.


Hata hivyo amekanusha madai ya kuwa kipindi mikutano ya siasa imezuiliwa hapa nchini,  chama cha mapinduzi (CCM)  kiliendelea mikutano hiyo kama kawaida na kusema kilichokuwa kinafanyika ni ukaguzi wa ilani pekee na siyo mikutano ya hadhara kama inavyodhaniwa.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI