Header Ads Widget

DR MPANGO: VIONGOZI WA SERIKALI WANACHANGIA KWA KIASI KIKUBWA UHARIBIFU WA MAZINGIRA

 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango amesema wapo baadhi ya viongozi ambao kwa maslahi yao binafsi wanachangia uharibifu wa mazingira na kwamba haamini kama kuna maskini mwenye uwezo wa kuingia katika vyanzo vya maji akiwa na zaidi ya mifugo 3000

 

Dkt. Mpango, amesema hayo leo Desemba 19, 2022 katika Kongamano la Wahariri na Wadau wa Uhifadhi, Mazingira na Utunzaji wa vyanzo vya maji, na kusema viongozi wa namna hiyo hawafai kwa kuwa wanaweka rehani maisha ya watanzania na kwamba Serikali haiwezekani kuacha tabia hiyo iendelee kwakuwa ina madhara kwa jamii.

 

Awali, Mwenyekiti wa jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile, alipopata nafasi ya kuzungumza alisema yupo tayari kutoa majina ambayo ni familia 12 zinajimilikisha eneo katika bonde la Usangu kinyume cha sheria na kupelekea maeneo mengine kukosa maji.

 

Balile amedai ndani ya familia hizo wamo baadhi ya wabunge, majaji, mawaziri na baadhi ya viongozi wengine wa serikali.

 

Mwenyekiti wa Kituo cha Wanahabari Watetezi wa Rasilimali na Taarifa MECIRA, Habibu Mchange amesema kuwa shughuli za kibinadamu zinazofanywa na wananchi wachache katika bonde la Ihefu ndio wamekuwa chanzo cha kukauka kwa Mto Ruaha.

 

Mchange amesema, kutokana na uharibifu huo kumepelekea wanyama wengi katika hifadhi ya Taifa Ruaha kufa na wengine kuambukizwa magonjwa mbalimbali kutokana na kukosa maji ya kutosha.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



BBC NEWS