Header Ads Widget

NG'OMBE ZAIDI YA 375 WAKAMATWA NDANI YA HIFADHI YA RUAHA.


Ng'ombe zaidi ya 375 wamekamatwa ndani ya  Hifadhi ya Ruaha katika Bonde la Usangu /Ihefu majira ya saa mbili usiku Jana Tarehe 07/11/2022 ,Hii ni mbinu Mpya ya wafugaji  kuingiza Mifugo usiku  wakiamini askari wa uhifadhi watakuwa wamelala.


Akizungumza na waandishi wa habari kwenye kituo cha Ikoga Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya Afisa Uhifadhi  wa TANAPA Benedict  Mwageni amesema Jeshi la Uhifadhi litafanya  kila jitihada ya kuhakikisha shughuli za kibinadamu hazifanyiki katika bonde hilo


Mwageni amewataka  wananchi waache kuingiza mifugo ndani ya  hifadhi kwa kuwa nchi iko kwenye mgao wa umeme unaosababishwa na Mto Ruaha kukauka pamoja na  wanyama kukosa maji jambo linalopekea vifo 


Hata hivyo Ng'ombe hao waliokamatwa wanasubiri kutambuliwa na Wafugaji huku taratibu za kisheria zitafuatwa ikiwemo kufikishwa mahakamani.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI