Header Ads Widget

WAZEE MBARALI WALALAMIKIA KUTWISHWA MZIGO WA KULEA WAJUKUU

Na Matukio daima media , Mbarali

KUELEKEA maadhimisho ya siku ya wazee duniani baraza la wazee wilayani Mbarali mkoani Mbeya  limewaomba vijana  kuwapunguzia mzigo wa kulea wajukuu bila sababu  za msingi hali inayopelekea wazee hao kuelemewa na mzigo wa kulea  licha ya vijana kuwa na nguvu za  kutosha .

Hayo yamesemwa jana na Katibu Msaidizi  wa Baraza la wazee wilayani humo ,Christina Mwalyaje wakati akizungumza na mtandao huu  jinsi walivyojipanga kuelekea maadhimisho ya siku ya wazee duniani ambayo hufanyika tarehe 1/10/2022 kila mwaka kama sehemu  ya kuleta usawa na  kuboresha maisha ya wazee.


Mwalyaje alisema kuwa kwa wilaya ya mbarali maadhimisho hayo yamepangwa kufanyika kwa ngazi ya katika kata ya Igurusi ambapo ujumbe  wa maadhimisho hayo ni “Ustahimilivu na mchango  wa wazee ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa”.

“Umri wetu sisi wazee tumechoka sana lakini sasa tunatwishwa mzigo  mkubwa wa kulea wajukuu na ukiangalia wengine hatuna nguvu tena za kuhangaika na wajukuu hivyo tunaomba vijana watupunguzie mzigo kwani kwa umri huu tulionao tunahitaji kupumzika na sio kuhangaika tena “alisema Mwalyaje.

Hata hivyo Katibu huyo aliwaomba viongozi wa dini  kusherekea sikukuu hiyo muhimu pamoja na wazee kwa kuendelea kuwaombea wazee wote afya njema,kufanya ibada maalum kwa ajili ya wazee wa Taifa ndani ya nyumba za ibada pamoja na kuelimisha waumini juu ya uzee na maandalizi ya uzee na kuzeeka.

Mwalyaje alisema kuwa faraja nyingine ambayo wanapaswa kupatiwa wazee  ni misaada ya chakula, nguo,dawa na mahitaji mengine muhimu kwa wazee wanaoishi katika hali ya umaskini uliokithiri.

Alisema kuwa kitu kingine wanachopaswa kuwasaidia wazee ni kuomba waumini wa dini mbali mbali kuendelea kuwasaidia wazee  wanaoishi  pekee yao katika umaskini mkubwa  na wazee wengine wenye uhitaji .

“Lakini tunawaomba waumini Kuwakumbusha  kuwalinda wazee wanawake dhidi ya mila na desturi zilizopitwa na wakati,wazee wanapaswa  kulindwa ,kulelewa na kutetewa  dhidi ya vitendo vya ukatili pamoja na kuwaonyesha upendo  na faraja”alisema.

Akizungumzia kuhusu miundo mbinu ya kwenye nyumba za ibada Katibu Mwalyaje alisema nyumbza za ibada zote ziendelee kujenga miundo mbinu rafiki kwa  wazee  walemavu ili waweze kushiriki ibada vizuri.

Meneja miradi wa Shirika  lisilokuwa la kiserikali linalojishughulisha na masualaya wazee wilayani Mbarali (KIWWAUTA),Moses Nchimbi alisema wanashirikiana na mabaraza ya wazee na Halmashauri ya wilaya ya mbarali katika kufanya maadhimisho hayto ya wazee  kwa ngazio ya kata kuanzia septemba 21 kwa tarehe tofauti m paka October mosi mwaka huu siku ya kilele.

“Kazi kubwa ambayo pia tumekuwa tukifanya ni kuhamasisha wazee  kuendelea kupata chanjo ya  Covid-19 kupitia mabaraza yao ya vijiji ambayo yapo katikla maeneo mbali mbali bado tunawapatia wazee elimu ya kujinga na Covid 19 kama inavyoelekezwa na wizara ya Afya na na shirika la afya duniani (WHO)”alisema.

Hata hivyo Nchimbi alisema kuwa shirika hilo limekuwa mstari wa mbele katika kusaidia wazee wilayani humo  pamoja na kusimamia masuala mbali mbali ya  kwenye jamii ambayo yanakuwa  yanawakabili .

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI