Header Ads Widget

TAMASHA LA CHOMA CHOMA FESTIVAL NI LEO TANGA

 


Wakazi wa jiji la Tanga wanatarajia kuongeza maeneo ya kuburudika kwa tamasha la chomachoma festival litakalozinduliwa Leo  September 10,2022 katika viwanja vya Mwahako jijini Tanga


Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Halmashauri la jiji la Tanga,Mwnyekiti wa chama cha chomachoma festival,Elizabeth Chawenda  alisema tamasha hilo litakuwa likifanyika mara mbili mwezi


Alisema kwamba kwenye tamasha hilo kutakuwa na aina zote za Nyama ikiwemo ya ngo'mbe,mbuzi ,kuku na samaki


Chawenga alisema Tamasha hilo litakuwa linafanyika kila juma most na juma pili ya mwezi kuanzia asubuhi mpaka usiku kwa lengo kuwapatia fiursa wakazi wa Tanga ya kupumzika baada ya kazi za wiki nzima


Hata hivyo,Chawenda alifafanua kuwa kutakuwepo na burudani mbali mbali ikiwemo ngoma mziki mnene  na michezo kwa watoto 


Alisema kutakuwa na vinywaji vingi na vya aina zote  ikiwa ni pamoja na vinywaji laini na vikali


"Nawaomba wakazi wa Tanga wafike kwa uwingi wao ili kufanikisha shughuli hiyo ya aina yake"alisema Chawenda ambae pia ni Meneja wa NMB Bank Mkoani Tanga


Pia alitoa wito kwa wakazi wa Wilaya za jirani ikiwemo Muheza,Mkinga na Panga I kujitokeza kwa wingi kuja kujumuika na wakazi wa jiji la Tanga katika starehe hii isiyo na kiingilio


Tamasha hilo la aina yake linatarajiwa kuzinduliwa na mgeni rasmi ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Tanga,Hashim Mgandilwa katika viwanja vya maonyesho ya biashara Mwahako jijini Tanga


Tanga choma choma Festival limedhaminiwa na taasisi ya SIDO,SELF Micro Finance,Tanga jiji na wenyeji  NMB ambae ndie mratibu wakuu wa Tanga choma choma Festival.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI