Header Ads Widget

MALORI YENYE UZITO MKUBWA JANGA KUBWA BARARABA YA LAMI SAWALA ,LUHUNGA NA IYEGEA MUFINDI ...

 

Ijazaji huu za mazao ya misitu ni hatari Kwa barabara ya lami kati ya Sawala, Luhunga na Iyegea wilaya ya Mufindi mkoani Iringa
Hili ni eneo lililoharibiwa na Lori ambalo lilizidisha mzigo na taili kupasuka hivyo kutembelea lim 

WANANCHI  wa vijiji  vya  Sawala ,Luhunga na Iyegea  katika wilaya ya  Mufindi  mkoani  Iringa wamepongeza  ujenzi  wa  wa barabara ya kiwango cha toka Sawala, Mkonge, Igoda, Ikaning'ombe na yegeya kuwa  umesaidia   sana  kero ya  usafiri japo  wameomba serikali kuwabana  wanye malori yanayobeba mizigo  mizito  kupita uwezo wa barabara  hiyo .

Wakizungumza na matukio  Daima App  juzi  wananchi hao   walisema pamoja na  jitihada  kubwa   zinazofanywa  na  serikali na  wahisani  kujenga barabara  hiyo  kwa  kiwango   cha lami  ila changamoto  kubwa  wanayoiona ni malori ya mazao ya  misitu  ambayo baadhi yamekuwa chanzo cha  kuharibu  barabara  hiyo .

Frank Ndelwa  mkazi wa  Luhunga  alisema   ili  barabara  hiyo  iendelee  kuwa  bora  ni vema  kuwepo kwa  sheria kali kwa  wamiliki wa malori yatakayobainika   kuzidisha mizigo na  kupita kwenye  barabara  hiyo .

Kwani  alisema kampuni  za  ujenzi  ambazo  zinaendelea  kufanya kazi ya  kukamilisha ujenzi hiyo pamoja na  kufanya kazi kwa  kiwango  ila kama hakutakuwa na usimamizi na sheria kali  za  kulinda miundo mbinu ya barabara  hiyo kazi hiyo  itakuwa ni bure maana muda  mfupi barabara  itakuwa imeharibika .

Ajuaye  Sanga mkazi wa  Sawala  na  mwisho  kijiji  cha Iyegea alitaka mwanzo wa  barabara  eneo la  Sawala kuwepo  kwa  tangazo linaloonesha  gari tani ngapi  linatakiwa  kupita kwenye  barabara  hiyo na aina ya adhabu ambayo itatolewa kwa mkiukaji wa  agizo   lililowekwa .

Kuwa kazi ya  kusimamia sheria   hiyo  inapaswa  kufanywa na serikali  za  vijiji  vyote  vinavyopita  barabara  hiyo  ili  kuona miundo  mbinu ya  barabara  inalindwa na  barabara  inabaki kubwa  mkombozi wa  wakulima wa mazao mbali mbali yanayozalishwa na wakulima  wa ukanda  huo kama  miti ,chai  na mazao  mengine ya  chakula.

Alisema barabara hiyo itakuwa ni mkombozi kwa wakulima wa chai waliokuwa wakipoteza mazao yao kwa kushindwa kufika kiwandani kwa wakati kutokana na ubovu wa barabara hasa kipindi cha masika


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI