Header Ads Widget

KESI YA MAUAJI YA MAOFISA WA MAGEREZA YAZIDI KUPIGWA KALENDA

 



Na HADIJA OMARY _LINDI


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Lindi imeendelea kusogeza mbele kesi ya mauwaji inayowakabili Maofisa watatu wa Magereza Mkoani Lindi akiwemo Mkuu wa Gereza la Liwale Mkoani humo SP Gilbert Sindani  na kupangwa kusikilizwa tena Augost 15 mwaka huu kutokana na ushahidi wa kesi hiyo kuto kamilika 



Hii ni mara ya nne  kwa watuhumiwa hao kufikishwa Mahakamani hapo ambapo kwa mara ya kwanza walifikishwa Mahakani juni 23 ,2022 na leo wamefikishwa Mahakamani na kesi yao kuhailishwa mpaka August 15  mwaka huu huku watuhumiwa wa kesi hiyo wakilazimika kusalia rumande




Watuhumiwa wengine wa kesi hiyo ni pamoja na Sajent yusuph Athumani na Coplo Fadhili Afwad wote ni maofisa wa gereza la Liwale 



Kesi hiyo yenye namba RMPI 1 ya  mwaka 2022 iko chini ya Hakimu   Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa wa Lindi Consolatha Singano  imesikilizwa kwa mfumo wa kimtandao ambapo baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Mwanasheria  wa Serikali kuwa upelelezi wa kesi hiyo ya Mauaji kutokamilika ndipo akaipangia tarehe nyingine ya kusikilizwa.




Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI