Header Ads Widget

POLISI WA AFRIKA KUSINI KUFANYA UCHUNGUZI KWENYE MABAA BAADA YA VIFO KUTOKEA

 

imu za uchunguzi zinafanya uchunguzi katika eneo la tukio
Image caption: imu za uchunguzi zilichunguza kilichotokea kwenye eneo la tukio

Polisi wa Afrika Kusini Jumatatu walikuwa wakifanya uchunguzi katika baa ambapo vijana 21 walifariki kwa njia isiyoeleweka huku manusura wakielezea vita vya kutoroka eneo lililokuwa limejaa msongamano wa watu huku mtu mmoja akisema kulikuwa na ukosefu wa hewa safi.

Wengi wa wahasiriwa, wengine wakiwa na umri wa miaka 13, walipatikana wamefariki ndani ya baa maarufu katika jiji la kusini mwa London Mashariki.

11 walifariki dunia ndani ya baa hiyo, huku wanne wakifia hospitalini.

Wengine 31 walilazwa hospitalini wakiwa na dalili zikiwemo maumivu ya mgongo, vifua kubana, kutapika na maumivu ya kichwa, afisa alisema.

Wengi waliruhusiwa kuondoka hospitali siku ya Jumapili huku wengine wawili wakisalia hospitalini, walisema.

Bw Cele, ambaye alitembelea eneo la tukio na kupewa taarifa na polisi wa eneo hilo, alisema waliofariki walikuwa na umri wa kati ya miaka 13 na 17 - lakini orodha ya kina ya wahasiriwa wakati huo haikuwa imetolewa.

Umri wa chini wa kisheria wa kunywa pombe nchini Afrika Kusini ni miaka 18.

Kuna ripoti kwamba watu waliokuwa wameenda kujivinjari walikuwa wakisherehekea mwisho wa mitihani ya shule.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI