Na Hamida Ramadhan Matukio Daima APP Dodoma
MWANAFUNZI wa kiume wa kidato cha kwanza mweye umri wa Miaka 15 anayesoma katika shule ya sekondari Chikole iliyopo mkoni Dodoma amelawitiwa na Mwanaume mwenye umri wa miaka kati ya 35-40 wakati akiteka maji kwenye Bwawa kwaajili ya kusafisha darasa
Tukio hilo limetokea mnamo Aprili 1,2022 majira ya saa 6:00 mchana katika Bwawa mtaa wa Senje Kata ya Msalato mkoani hapa.
Akizingumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Onesmo Lyanga amesema mtuhumiwa huyo ametenda kosa hilo baada ya kuwakamata wanafunzi watatu walio kuwa wakichota maji kwa ajili ya usafi wa darasa huku akiwatishia kuwaua kwa panga kisha kumlawiti mmoja wao.
‘’Kwa bahati mbaya walikuwa wanafunzi sita walikuwa wameenda kuchota maji katika hilo Bwawa na wakaweza kukutana na mtu mmoja ambaye wao wanamtambua kwa sura na waajiri wake.
Na kuongeza "Mtu huyo ameweza kuwatolea vitisho na kuwauliza maswali,kwanini wanateka maji hapo? na akawauliza wale ambao ni mara yao ya kwanza kuteka maji katika Bwawa hilo wakatokea wanafunzi watatu wakamjulisha kwamba wao ni mara yao ya kwanza akawaambia nyinyi nendeni .’’ amesema Lyanga
Amendelea Kusema"Lakini akawachukua wanafunzi watatu huku akiwa na kitu kama panga na kuwatisha baada ya kufanya hivyo aliwachukua na Kwenda nao katika vichaka na ndipo huko alipo weza kufanikiwa kumlawiti mwanafunzi mmoja kati ya hao watatu.’’ amesema Lyanga
Aidha, Lyanga amesema mhanga wa tukio hilo kwa sasa anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma
"Uchunguzi zaidi unaendelea wa kumtafuta mtuhumiwa na kumbaini Lakini niagize na kumtaka mtuhumiwa ajisalimishe haraka kwa kuwa anatambulika kwa sura.’’ anasisitiza Lyanga
0 Comments