Mtendaji mkuu wa ASA,Dkt Sophia Kashenge akikangua mbegu bora zinazalishwa na wakala
Na Lucas Raphael Dodoma
WAKALA WA MBEGU NCHINI ASA WATAKIWAA KUTOA ELIMU YA MATUMIZI YA MBEGU BORA
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo,Prof Siza Tumbo amewataka Wakala wa Mbegu nchini ASA ,kuhakikisha wanatoa elimu ya matumizi bora ya mbegu kwa wanunuzi na wakulima ili kuongeza asilimia ya watumiaji wa mbegu bora
zinazosambazwa na wakala huyo nchini
Alitoa Kauli hiyo alipokuwa akifungua kikao kilichofanyika katika ukumbi wa wizara ya Kilimo Dodma baina ya Wakala wa mbegu nchini (ASA) na wasambazaji walioingia mkataba wa kusambaza mbegu na wakala huyo,
Alisema kwamba Wakala anapaswa kuongeza jitihada katika usambazaji ili kuongeza idadi ya wakulima wanaotumia mbegu bora.
Prof Tumbo alisema takribani asilimia 10 ya wakulima wanaotumia mbegu
bora ambazo zimeboreshwa hivyo wasambazaji wa mbegu mnapaswa kuwa
maafisa ugani kuwaelimisha wanunuzi umuhimu wa matumizi ya mbegu
bora,jambo litalaochangia kuongeza uzalishaji wenye tija kwa wakulima
kwa kutumia mbegu bora za mazao.
“Ni asilimia chache ya wakulima wanaotumia mbegu bora za wakala wa
uzalishaji mbegu,hivyo mnapaswa kuongeza bidii ya kusambaza mbegu kwa
wakulima pamoja na kuwapa elimu ya kuzitumia,”alisema Naibu Katibu
Mkuu.
Alifafanua zaidi ya kuwa idadi ya watumiaji wa mbegu bora
ikiongezeka,basi hata soko litakuwa kubwa kwa wakulima kutokana na
kwamba,wakulima hao watakuwa na uzalishaji wa kutosha katika mashamba
wanayozalisha mbegu hizo.
Prof Tumbo akizungumzia kuhusu uzalishaji wa mazao wenye tija ambao unaleta matokeo chanya,alisema mkulima anatakiwa kuwa na viauatilifu,mbolea,mbegu bora na vitu vingine ambavyo vitamsaidia
mkulima kuboresha shamba lake kabla na baada ya msimu wa mavuno.
"mpaka leo hii bado wakulima wanahangaika na uzalishaji wa
mahindi kutokana na kutofuata taratibu za kilimo bora kitendo
kinachochangia kupata tani chache za mahindi kwa heka moja ya
shamba,ukilinganisha na mkulima anayefuata matumizi bora ya kilimo "alisema Prof Tumbo.
Alisema,wakulima wakizingatia kufuata kanuni bora za kilimo,watasaidia kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa uzalishaji wa mbegu bora ambazo zitaleta tija kwa taifa na wananchi kwa ujumla.
Alisema serikali kila wakati wanasisitiza suala la matumizi ya mbegu bora ,Viuatilifu zana za kilimo kwa sababu vitu hivyo ukiwa navyo na wakijua kuvitumia vizuri wanaweza kupata mazao yale ambayo tunasema wanazalisha kwa tija.
Naye Mtendaji mkuu wa ASA,Dkt Sophia Kashenge alisema maelekezo waliopewa na Wizara watayafanyia kazi kikamilifu ikiwemo kuhimiza wadau
wasambazaji wa mbegu katika maeneo ya pembezoni kuongeza bidii ya
kuwafikishia wakulima kwa wakati wote hasa msimu wa Kilimo
Alisema moja ya changamoto ambayo inawasumbua wakulima ni
ucheleweshaji wa mbegu,hivyo hilo watalifanyia kazi ili kuhakikisha
wanaboresha hilo,ambalo anaamini litasaidia kutatua changamoto .
Hata hivyo alisema kikao hicho na wadau wasambazaji wa mbegu ambao
wameingia mkataba wa kusambaza mbegu kwa wakulima,kitasaidia
kuimarisha Ushirikiano baina yao,kutokana na kwamba sasa hivi serikali
imeelekeza nguvu katika kufanya kazi na sekta binafsi.
“Tunaishkuru serikali kwa kuamua kufanya kazi kwa karibu na sekta
binafsi,hili litaongeza ufanisi katika usambazaji wa mbegu,”alisema Dkt
Kashenge.
Alisema wanapofanya kazi pamoja na sekta binafsi,wanaongeza wigo wa
utendaji,ambapi kiu yao ni kuhakikisha usambazji wa mbegu
unaongezeka kwa kiasi kikubwa ili mkulima asipate tabu ya kupata
mbegu,pindi msimu wa kilimo unapowadia.
0 Comments