SHIRIKA la umeme Tanzania (TANESCO ) mkoani Iringa limeanzisha oparesheni maalumu ya kuwawaingizia umeme wateja zaidi ya 2170 ambao walilipia gharama ya Tsh 27000 kabla ya gharama mpya za umeme kutangazwa .
Afisa mahusiano wa TANESCO mkoa wa Iringa Francis Mbwele alisema kuwa zoezi hilo linatekelezwa na kikosi kazi kilichoundwa na TANESCO mkoa wa Iringa kutoka wilaya ya Mufindi , Kilolo na Iringa ili kuhakikisha wateja wote walioomba huduma ya umeme wanaingiziwa umeme kabla ya Machi 31 mwaka huu.
“ Tunachokifanya sasa ni kutekeleza agizo la serikali la kuhakikisha kabla ya Machi 31 mwaka huu wateja wote wawe wameunganishiwa umeme na baada ya zoezi hilo kumalizika TANESCO mkoa wa Iringa imejipanga mteja wake mpya baada ya maombi ya kukamilisha kujaza fomu ndani ya wiki mbili atakuwa ameunganishwa na huduma ya umeme”alisema
Alisema kuwa idadi kubwa ya wateja ambao waliomba umeme ilikuwa Iringa mjini na Kihwele ambako TANESCO imepeleka kikosi kazi cha kukamilisha uingizaji wa umeme kwa wateja wake na baada ya kumaliza huko kikosi hicho kitaelekeza nguvu zake maeneo mengine ili wateja wote kupata huduma hiyo kama walivyo omba.
Alisema kuwa changamoto iliyokuwa ikikwamisha wateja kuunganishwa umeme kwa wakati ilikuwa ni upatikanaji wa vitendea kazi ambavyo kwa sasa vipi vya kutosha na wana uhakikia mkubwa wa kutekeleza majukumu yao kwa wakati .
Alisema kuwa upungufu wa vifaa ulisababishwa na ongezeko kubwa la wateja wa umeme ambao walijitokeza kwa wingi baada ya gharama ya kuingiza umeme ilikuwa ya chini zaidi mjini na vijijini ila kwa sasa kasi ya wateja wapya siku kubwa sana imerejea ile ya awali ambayo wana uhakika mkubwa wa kufikisha huduma hiyo kwa wakati zaidi .
Hata hivyo Mbwele aliwataka wananchi wanaohitaji huduma ya umeme kuendelea kujitokeza kwani uhakika wa kuunganishwa na umeme upo mkubwa na ndani ya muda mfupi baada ya maombi mteja atakuwa ameunganishiwa umeme.
Kwa upande wake mhandisi mkuu wa TANESCO mkoa wa Iringa Twaha Kisaka alisema kuwa tayari serikali imetoa muda wa kukamilisha zoezi hilo la ndio sababu ya kutengeneza timu za kazi ili kukamilisha zoezi hilo ambapo timu 13 zimeundwa na kila timu kwa siku itatengeneza service line 20 kwa simu na kwa timu 13 watajenga zaidi ya service line 200.
Alisema kuwa wateja wote wanaoingiziwa umeme halina gharama mpya kwa wale ambao walilipia kiasi cha shilingi 2700 wataingiziwa kwa gharama hiyo hiyo ambayo walilipia wakati huo hakutakuwa na gharama mpya na wale wanaoendelea kulipia kwa gharama mpya nao watafikishiwa umeme kulingana na walivyolipia.
Mteja mpya wa umeme mkazi wa Kitwiru Iringa Amina Sanga alisema toka mwaka 2021 alipohamia katika makazi yake mapya eneo hilo hakuwa na huduma ya umeme na kuwa zoezi hilo la kuanza kuwaingizia umeme wateja wapya kwake ni fursa kubwa .
Hivyo alilishukuru shirika la umeme kwa kazi hiyo nzuri ya kuwafikia wateja wake wapya na kuwa kufikishwa kwa huduma hiyo ya umeme ni mwanzo mwema wa wananchi kukuza kipato chao kwa kuanzisha shughuli za uzalishaji kupitia umeme.
Mary Kususange mwenyekiti wa mtaa wa Kitwiru B pamoja na kupongeza TANESCO kwa oparesheni hiyo ya kuwaingizia umeme wateja wapya bado aliomba utekelezaji wa zoezi hilo uwe shirikishi kwa wenyeviti wa mitaa ili waweze kuwaonesha maeneo yenye uhitaji mkubwa wa umeme.
Alisema mtaa wake una maeneo ya pembezoni zaidi ambayo wananchi wake bado kufikiwa na nguzo za umeme hivyo kutokana na bei mpya ya umeme TANESCO waangalie uwezekano wa kusogeza nguzo jirani na makazi ya wananchi hao ili waweze kuingiza umeme .
0 Comments