Na Ibrahim Kunoga Tanga.
Mbunge wa Lushoto Mh Shabani Shekilindi ameiomba serikali kupiga marufuku uchimbaji wa madini katika maeneo ya Kwemashai na Magamba katika wilaya ya Lushoto.
Kauli hiyo ameitoa katika kikao cha bajeti cha kamati ya ushauri wa mkoa wa Tanga.
Mh shekilindi ametaka kikao hicho kiamuae na kupiga marufuku maeneo hayo madini yasichimbwe ili kuokoa mazingira na kuomba watoa leseni wasitishe kutoa leseni.
Pamoja na hayo mh shekilindi amesema kuna maeneo yanaitwa madhahabu ambapo watu wanachimba dhahabu kwenye vyanzo vya maji hali inayopelekea watu waishio mabondeni kukosa maji.
"Mimi ushauri wangu maeneo Yale yasitishe kabisa yasichimbwe madini kwa sababu yakichimbwa milima itaporoka na yapo maeneo hatarishi ikiwemo shule na makazi ya watu;Amebainisha Mh Shekilindi.
Kutokana na kutegemea vyanzo vya maji vinavyotoka maeneo hayo Mbunge huyo amesema kwa sasa vita vya tatu vitakavyotokea vya athari ya dunia itakuwa ni maji .
Pia amesema kwa sasa maeneo mengi lushoto watu wamechoma misitu lakini maeneo hayo hayajawahi kurudishiwa miti na kuomba wataalam walishughulikie ili mapato yaongezeke na mazingira yaweze kuboreshwa.
Sambamba na hayo amesema pia wilaya hiyo umeme unahitajika sana kuboreshwa ili kuongeza mapato na kusema kuwa wananchi wengi wa lushoto wanategemea umeme ndio maana huwezi kukuta nyumba ya nyasi kwa hiyo umeme utakapofika vijijini tayari mapato ya halmashauri yataongezeka.
0 Comments