Mkuu wa jeshi la Polisi nchini
JESHI La polisi linamshikilia mwanadada Neema Mwambusi Uswege (29) mkoani mwanza kwa kosa la kumlisha mama mkwe wake sumu kwenye chakula nakumsababishia umauti. Inadaiwa kuwa mama wa James Bulaya (38) Aneth Manyirizu umemkuta umauti huo tarehe 13/1/2022 saa 12:00 mchana alipopelekwa hospital baada ya kutapika damu nyingi nakupoteza uhai, Aneth
Manyirizu amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 79 katika hosipital inayodaiwa siyo ya kiserikali hata hvyo uchunguzi wa polisi umedhibitisha kuwa Neema Mwambusi Uswege Wege ndie mtuhumiwa mkuu kwani watoto wake walitowa maelezo kuwa mama ndye alimpikia chakula bibi yao nakuwakataza wasije wakathubutu kula chakula kile.
Watu wajirani wametowa maelezo kuwa ugomvi wao na mumewe ulikuwa ukijirudia mara kwa mara huku mwanamke alikuwa akimjibu mumewe kuwa yeye kwake siyo kituo cha kulelea wazee tofauti na hvyo atarudi kwao mbeya.bwana James ni mfanyabishara mkubwa wa dagaa tz na nje ya nchi amesikitishwa kwa tukio hilo la kufiwa mama yake ambaye ndye mzazi pekee aliebaki
0 Comments