Header Ads Widget

WANANCHI HAWANA ELIMU YA JINSI YA KUJIKINGA NA KIFUA KIKUU

 

Watanzania 73  hufariki Kila Siku kutokana na ugonjwa wa kifua kikuku ambayo imeonekana idadi hiyo ni kubwa ukilinganisha na wanawake wajawazito.Mwandishi Rehema Abraham


Amesema hayo mganga wa hospitali ya maalum ya magonjwa ambukizi  kibongoto  Drt. Leornard Subi iliyopo Siha mkoani Kilimanjaro wakati alipokuwa akiongea katika katika zoezi la uzinduzi wa Afya marathon  inayotarajiwa kufanyika tarehe 26 mwezi wa 12  iliyoambatana na zoezi la upandaji miti katika hospitali hiyo.

aidha amesema kuwa ugonjwa huo umekuwepo kwa chini chini lakini inaongoza kwa kuuwa watu mbalimbali Kila Siku na hiyo inatokana na watanzania kutopewa   elimu juu ya ugonywa huo.


Sambamba na amewapongeza wadau waliokuja na mpango wa Siha marathon agenc itakayosaidia  kutoa elimu kwa wananchi na kusema taasisi za Serikali na zisizo za Serikali zishirikiane katika kuelimisha wananchi juu ya mapambano ya ugonjwa wa  kifua kikuu.

"kwa bahati mbaya ugonjwa wa Kifua kikuu unawathiri watu wanaoishi kwenye familia duni ,watu waliopo kwenye migodi ,maeneo ya magereza,misongamano na kwa bahati mbaya Sasa Kuna baadhi ya wagonjwa wanaoupata usugu wa madawa na ndio maana tunajenga maabara ya kisasa ,na kuendeleza sayansi ya kitafiti na uchunguzi "Alisema.

Amesema kuwa mbio hizo za marathon zomeambatana na ujumbe wa afya ya namna gani ya kuweza kutokomeza ugonjwa wa kifua kikuu 

Amesema kuwa ugonjwa wa kifua kikuu ni ugonjwa wa muda mrefu na sio kitu kipya kwani hospitali hiyo ya kibongoto ilianzishwa mwaka 1926 ambapo mwaka 1952 ikapewa fursa ya kuwa hospitali ndani ya wilaya hiyo.


Akizungumza wakati wa ugawaji wa miche hiyo  Mwenyekiti  wa taasisi ya Siha Sports Agency Sellina Mkonyi  amesema  kuwa ili kuendana na dhima ya mbio izo za Siha Afya marathon  jamii inapaswa kuwa mstari wa mbele kwenye utunzaji wa mazingira ukizingatiwa kipindi  hikili chenye ukame kwenye maeneo mengi  kwa ukataji wa miti ovyo na uharibifiu wa vyanzo vya maji kwani miti 3,000 itapelekwa hospitali ya Kibong'oto na 5,000 itaoteshwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Siha.

Katika kuelekea  madhimisho ya Siha Afya  Marathon Wakala wa  Misitu (TFS) wametoa miche  8,000,ambapo miche 3,000 itapandwa kwenye hospitali ya Kibong'oto na maeneo mengine ili kutunza mazingira katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Kilimanjaro.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI