Header Ads Widget

MAANDALIZI YA TAMASHA LA UHURU BONANZA YAKAMILIKA KWA 90%

 




Na Pamela Mollel,Monduli


Tamasha kubwa la uhuru bonanza linalotarajiwa kufanyika Wilayani Monduli siku ya Jumamosi  wiki hii maandalizi yake yamekamilika kwa zaidi ya asilimia 90


Wakizungumza  na waandishi wa habari  waandaaji wa Bonanza hilo wakiongozwa na Mwenyekiti wao Costastine Shayo  anasema tamasha hilo limeandaliwa na wadau wa michezo lenye lengo la kuibua vipaji pamoja na kusheherekea miaka 60 ya uhuru


Alisema kuwa mpaka sasa maandalizi ya bonanza hilo yamekamilika kwa zaidi ya asilimia 90 ambapo yameshirikisha chama cha soka na chama cha riadha 



Katibu chama cha Mpira wa miguu Monduli Abubakary  Hamis alisema kuwa kupitia bonanza hilo litaweza kuitangaza vyema wilaya hiyo




Hapo katika wilaya yetu ya Monduli kuna watu mashuhuri ambao walishatumikia taifa hili lakini pia tuna vivutio vingi"alisema Hamis


Aliongeza kuwa bonanza hilo litaleta chachu katika michezo hasa kwa upande wa wanawake ikizingatiwa wilaya hiyo ni jamii ya kifugaji



Msemaji wa Bonaza hilo Amir Mongi alisema kuwa zaidi ya wadau wa michezo 3000 wanatarajiwa kushiriki Mashindano haya ambayo  yatashirikisha mpira wa miguu,riadha, mbio za baskeli ,netbol,pamoja na kukimbiza kuku


"Bonaza hili nilakukata na shoka nawaomba wadau wapenda michezo wajitokeze kwa wingi"alisema Mongi


 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI