Header Ads Widget

JESHI LA ZIMAMOTO MKOANI KAGERA LANUSURU MAISHA YA MTOTO MCHANGA.

 



Jeshi la zimamoto mkoani Kagera limethibitisha kuokoa maisha ya mtoto mchanga wa kiume  anayesadikika kuwa na umri wa siku mbili hadi tatu aliyetupwa chooni katika shule ya msingi Rukajange iliyoko wilayani Karagwe mkoani Kagera......Na, Titus Mwombeki-MDTV BUKOBA.


Akiongea na Matukio Daima Media leo ofisini kwake kaimu kawanda wa jeshi la zimamoto mkoani Kagera Thomas Majuto amesema kuwa walipokea taarifa za tukio decemba mosi mwaka huu majira ya saa nnne na robo asubuhi baada ya kupokea taarifa ya tukio hilo kutoka kwa Mwananchi(hakutajwa majina) aliyekuwa anapita katika maeneo ya shule hiyo na  alisikia sauti ya mtoto mchanga  akilia kutokea  chooni na baada ya kupokea taarifa hizo ndipo jeshi la polisi wilaya ya Karagwe  liliwahi katika eneo la tukio na kweza kuokoa maisha ya mtoto huyo.


“ Baada ya kupokea waarifa za tukio hilo askari wa kituo cha zimamoto wiyaya ya Karagwe waliweza kukimbia mpaka katika eneo la tukio na kuanza kubomoa choo alipotupwa mtoto huyo na mwishowe walifanikiwa kumtoa  akiwa hai na kumkimbiza katika hospitali ya rufaa ya  Nyakahanga iliyoko wilaya ya Karagwe kwaajiri ya huduma ya kwanza na mpaka sasa mtoto huyo ameifadhiwa hospitalini hapo huku uchunguzi wa kumtafuta mama mzazi wa mtoto huyo ukiendelea ili aweze kufikishwa katika vyombo vya sharia”



Ameongeza kuwa kutokana na tukio hilo mpaka leo asubuhi wamepokea taarifa kuwa kuna mama mmoja ambaye ananyonyesha mtoto mchanga  amejitokeza  akiomba kumtunza mtoto huyo.


 “Tumeweza kufahamishwa pia, kuwa kuna mama mmoja anayenyonyesha amejitokeza akiomba kumtunza yule mtoto ili awe ananyonyesha watoto wawili na sisi kama jeshi la zimamoto mkoani Kagera wazo hilotumeliacha  kwa idara ya Ustawi wa jamii wilaya ya Karagwe walishughulikie ili waweze kutoa idhini na  huyu mama aweze kumchukua mtoto huyo ili  aweze kumpa huduma ya kumnyonyesha"


Aidha kamanda Majuto amewaomba wananchi mkoani Kagera kutoa taarifa kwa jeshi la polisi pale wanapoona mtu ambaye walikuwa wakimuona akiwa  na ujauzo au mtoto lakini mwishowe mtu huyo kuonekana  hana mtoto wala ujauzito ili kusaidia kutokomeza matukio haya.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI