Header Ads Widget

ULANGA WAFANYA MNADA WA KWANZA WA KOROSHO

Jumla ya shilingi 97,520,000. zimepatikana  kwenye  mnada wa kwanza kwa kuuzwa jumla ya tani 46 za korosho ambazo zimetoka wilaya za ulanga na malinyi mkoani morogoro. mwandishi wa matukio daima Jacob Sonyo anaripoti kutokea Morogoro

Hayo yalisemwa na afisa ushirika  halmashauri ya wilaya ya Ulanga Ester Mgaya, wakati wa kufanyika zoezi hilo la mnada ambapo alisema  jumla ya tani 46 sawa na kilo 46,000/= zilipelekwa kwenye mnada huo ambao  ndio mara ya kwanza kufanyika wilayani Ulanga ikishirikisha na Wilaya ya Malinyi.

Ester alisema kuwa wakulima wa wilaya hizi wanatakiwa kuwa na hali zaidi ya kulima zao hilo la Korosho kwani limeonekana kufanya vizuri katika wilaya hizi mbili Ulanga na Malinyi na kuachana na mazoea ya kilimo cha aina aina moja tu 

Naye   Afisa ubora  wa zao la korosho  Ahmad Salum  aliwataka wakulima kufuata maelekezo ya uandaaji wa korosho kwa kuzitenganisha zenye ubora ambazo ndizo zinazo takiwa kupelekwa sokono ili kuondoa usumbufu mara wanapofika sokoni hapo.

Aidha  wakulima wa korosho Wilayani Ulanga na Malinyi  waliishukuru Serikali kwa kuweza kuwapelekea  mnada  huo karibu nao ,ambapo umeweza kurahisisha juu ya uuzaji wa korosho zao na wamewaomba  Viongozi waweze kuwahimiza wanunuaji wa korosho kuwapelekea  fedha za malipo wa wakati.







Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI