Header Ads Widget

SIRI YA WANAWAKE NA NGUMI ZA KULIPWA NCHNI.

 


Kaimu Rais kamisheni ya  ngumi za kulipwa nchini  Agapeter Basil  amewataka wanawake kuingia katika mchezo huo ili kuleta chachu ya ushindani katika anga za kitaifa na kimataifa.


Akizungumza wakati  wa kufungua kozi ya waamuzi  wa ngumi za kulipwa  nchini yaliyofanyika  mjini  Morogoro  Basil amesema kuwa bado idadi ya wanawake Ni ndogo ikilinganishwa na wanaume katika mchezo wa masumbwi hivyo Ni fursa kwao kuendelea kujitokeza ili kuleta ushindani



Anasema katika mafunzo hayo  jumla ya wanafunzi wa ukocha 33 wanachukua mafunzo  wakiwemo wanaume 29 na wanawake 4 idadi ambayo ni ndogo .


Kwa upande wake katibu wa Chama Cha ngumi mkoa wa Morogoro  Joseph Ngalawa amesema lengo la kuanzisha kozi hiyo mjini Morogoro  Ni kuleta fursa kwa vijana  kupata ajira .


Ngalawa anasema kozi hiyo italeta chachu ya kukuza mchezo wa Masumbwi mkoani huo  na mpango ni kuandaa  mapambano  ya ngumi kila mwezi katika wilaya zote za mkoa huo ili kuibua vipaji vilivyopo vijijini.



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI