Header Ads Widget

IGP SIRRO APANGUA MA RPC , JUMA BWIRE NA MARISONE MWAKYOMA WAENDA MAKAO MAKUU ,ALLAN BUKUMBI AWA RPC IRINGA


IGP Simon Sirro 

 MKUU  wa   jeshi la  polisi nchini  (IGP) Simon  Sirro  amefanya   uhamisho   na mabadiliko kwa baadhi ya makamanda  wa  polisi  wa  mikoa nchini.

Taarifa  ya jeshi la  polisi iliyotolewa  leo Novema 10 2021    kupitia msemaji wa polisi inaeleza  kuwa  waliohamishwa  ni aliyekuwa kamanda wa  polisi wa  mkoa wa Iringa  kamishina  msaidizi  wa polisi (ACP) Juma  Bwire  ambaye  amehamishiwa makao makuu ya  polisi kamisheni ya  upelelezi wa makosa ya jinai na nafasi yake  imechukuliwa na aliyekuwa  afisa Mnadhimu wa mkoa huo  kamishina msaidizi wa  polisi (ACP) Alan Bukumbi.

Pia  aliyekuwa  mkuu wa oparesheni kanda  maalum ya  dae Salaam  Makame  Hamad  amehamishiwa  mkoa wa Katavi   kuwa kamanda wa  polisi wa mkoa  huo kuchukua nafasi ya kamishina Msaidizi  wa  polisi (ACP) Benjamin Kuzaga  ambaye  amekwenda  kuwa  kamanda wa  polisi wa mkoa wa Manyara .

 Pia  aliyekuwa  kamanda wa  polisi wa  mkoa wa Manyara  kamishina  msaidizi  wa  polisi   (ACP) Marisone Mwakyoma amehamishiwa  makao makuu ya polisi Dodoma  kuwa  msaidizi wa  ulinzi  wa  miundo mbinu muhimu  ya serikali  na kamishina msaidizi wa  polisi (ACP)  Zuberi Mwombeji  sasa anakuwa  mkuu wa   oparesheni kanda  maalum ya   Dar es Salaam .

 Taarifa  pia imeeleza  kuwa  mabadiliko  hayo ni ya kawaida  yenye  lengo la  kuboresha  ufanisi  katika  kutekeleza jukumu la jeshi la  polisi  la kulinda maisha ya raia na mali zao .

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI