Header Ads Widget

HALMASHAURI YA ULANGA YATOA MKOPO ZAIDI YA MILIONI 138 KWA MAKUNDI MAALUM.

 


NA MWANDISHI WETU , ULANGA MOROGORO


Halmashauri ya wilaya ya ulanga imetoa kiasi cha shilingi   138,185,000.00 na kuvikopesha jumla ya vikundi  24 vya vijana, akina mama, na walemavu  wilayani hapa


Akiwakabidhi hundi yenye thamani ya pesa hiyo mkuu wa wilaya ya ulanga  Ngolo Malenya amesema kuwa anamshukuru Rais wa Jamhuriya Muungano wa Tanzania Mh Samia  Suluhu Hassani kwa kuendelea kuwajali watanzania hasa kwenye mikopo isiyokuwa na riba



 Mh malenya amesema kuwa mikopo hiyo ni ya kisheria hivyo vikundi vilivyopata mikopo hiyo vinatakiwa kurejesha kwa wakati ili na wengine waweze kupata mikopo hiyo kama ambavyo wao walivyopewa


 Naye Kaimu Mkurugenzi Halmashauri  wilayani ulanga Juma Kapilima amesema kuwa katika kuhakikisha kuwa serikali ipo chini ya  Samia Suluhu Hassani mikopo hiyo kwa asilimia kubwa imetolewa kwa akina mama ukilinganishwa na akina baba 


Mbali na hilo Kapilima amewataka waliopata mikopo hiyo  kuhakikisha wanasaidia katika ukusanyaji wa mapato kwa kufichua wale wote wenye tabia ya kutorosha mapato ili halmashauri iwze kukusanya fedha ya kutosha na kuendelea kutoa mikopo hiyo.



Jumla ya vikundi 24 vimekopeshwa pesa hiyo ambapo  fedha yake imetoka katika vyanzo vya bakaa ya mwaka wa fedha uliopita 2020/2021 49,141,000.,makusanyo ya marejesho ya mikopo kiasi cha shilingi 31,500,000,na fedha zilizotengwa kutoka asilimia kumi ya mapato ya ndani kwa kipindi kuanzia mwezi julai hadi septemba 2021ni shilingi 57,544,000 nahivyo kufanya jumla ya fedha kuwa 138,185,000.


MWISHO

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI