Header Ads Widget

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA AAGIZA MAHAKAMA ILIYOHAMISHWA KURUDISHWA KIPONZERO

Naibu   waziri  wa  katiba na  sheria Geofrey  Pinda  akitoa maelezo  ya  kuhamishwa kwa mahakama ya  Mwanzo  Kiponzero kutoka  Ifunda  kwenda  Kiponzero , kutoka  kushoto  ni  diwani wa  kiponzero  Veny Mnyinga na mbunge wa Kalenga Jackson Kiswaga 
.................................
NAIBU  Waziri wa Katiba na Sheria Geofrey Pinda ameagiza  ndani ya mwezi  mmoja mahakama ya  mwanzo  ya tarafa ya  Kiponzero   wilaya ya  Iringa  iliyokuwepo   kijiji  cha  Kiponzero  kisha kuhamishiwa kijiji  cha Ifunda   kata ya  Ifunda  kurudishwa kata ya Kiponzero ambako inatambulika na si vinginevyo .

Akizungumza na  wananchi  wa Kiponzero  wakati wa  mkutano wa  hadhara  mara  baada ya  kutembelea majengo ya  yaliyokuwa yakitumiwa na mahakama ya mwanzo  kiponzero kabla ya  kuhamishiwa  Ifunda ,Pinda  alisema  utaratibu  uliotumika  kuhamisha huduma  za mahakama   hiyo  haukufuata  taratibu za  kiserikali  hivyo hadi sasa  mahakama  inayotambuliwa ni ya  Kiponzero na sio ya  Ifunda .

 Pinda  alisema  amefika  katika  eneo hilo la Kiponzero kujifunza zaidi  juu ya uamuzi  uliotumika  kuhamisha huduma  za mahakama katika  eneo hilo na  hadi sasa  amebaini  kuwa hakuna  taratibu  zozote za  kiserikali  zilizofuatwa  kuhamisha mahakama  hiyo  kwani majengo  yaliyopo Kiponzero ni majengo  yenye  sifa  zote za  kuendelea  kutoa huduma  za  kimahakama katika  eneo hilo .
Naibu  waziri wa  katiba ya  sheria  Geofrey Pinda  akiwa  jirani na mlango wa mahakam  ya Mwanzo  Kiponzero  iliyopo  Ifunda ,kulia ni katibu tawala wa  wilaya ya  Iringa Stomen Kyando 


Alisema  amekagua  jengo  linalotumiwa kama mahakama kwa  sasa  lililopo kijiji cha Ifunda  kuwa ni ni jengo  lisilo la  sifa  hata  moja ya  kutoma  huduma  za  kimahakama  kwani ni  jengo  ambalo halina  hadhi ya  kimahakama   tofauti na  jengo la Mahakama  lililopo  Kiponzero ambalo  limejengwa kwa  sifa za kimahakama .

Pia  alisema  kabla ya  huduma  za  kimahakama  kuhamishwa katika  eneo hilo ilipaswa kutolewa  tangazo  kwenye  gazeti la  serikali ila  kwenye  zoezi hilo la uhamishaji  wa mahakama    hiyo halijafanyika  na hadi sasa  wizara  inatambua  kuwa mahakama  ya  mwanzo  tarafa ya  Kiponzero  ipo  kijiji  cha  Kiponzero  na sio  kijiji cha Ifunda kama   ilivyo  sasa .

Alisema  kinachohitajika  katika  majengo ya mahakama  Kiponzero ni  kujenga  kituo cha  polisi  pamoja na kufanya ukarabati za  jengo   husika kwa  kupaka rangi  zoezi  ambalo  halitachukua  muda  mrefu .

" hata katika  mpango wa serikali wa  kuboresha  majengo ya mahakama   hatuwezi kuleta   fedha  kuja kukarabati jengo   hilo la Ifunda  ambalo ni jengo la  udongo na  kuacha   kwenda  kufanya  ukarabati  jengo la Kiponzero  ambalo  limejengwa  kisasa  mimi nafikiri   kama  ni hitaji ya  mahakama  eneo  hilo  ni kukaa kuangalia  ni  wapi  kwenye tarafa hiyo ya  kiponzero  kujengwe mahakama  nyingine  mpya ila  sio  kuhamisha huduma za  kimahakama katika  eneo la  Kiponzero"

Alisema  lengo la  serikali ni  kuhakikisha  kila  kata  inapata  mahakama  yake  ila mpango wa  sasa  kuelekea  2021/2026    wamepania  kuona kila makao  makuu ya tarafa kuna kuwa na mahakama  za  mwanzo .

Kuhusu changamoto ya  usafiri katika   mahakama   hiyo  alisema   serikali inajipanga  kuboresha   huduma  za  usafiri  katika maeneo  yenye  changamoto ya  usafiri  .

Awali  diwani  wa kata ya  Kiponzero Veni Myinga  alisema  kuwa   wananchi  wa  Kiponzero   wamekuwa  wakilalamikia suala   hilo  muda mrefu  kwa  zaidi ya miaka  15   sasa  toka mahakama   hiyo  huduma   zake  zilipohamishwa .

 Diwani   huyo  alisema  uamuzi  wa kurejesha  huduma  za kimahakama makao  makuu ya tarafa  ni  uamuzi  mzuri  ambao  utaondoa kero  kwa  wananchi  ambao  walikuwa  wakilazimika  kutembea umbali wa zaidi ya  kilometa 150 kutoka kijiji cha pembezoni kabisa mwa  tarafa ya  Kiponzero  kwenda kijiji cha  Ifunda  kufuata   huduma  za kimahakama .

Myinga  alisema  mahakama   hiyo ya  Kiponzero ni mahakama ya  kihistoria  kwani  ndio mahakama ya mwanzo kabisa kujengwa  na Chifu  Mkwawa   miaka  ya  1922 iliyopita na hadi sasa kwenye  jengo  hilo wamehama watu  ila nyaraka  zote  za kimahakama zikiwemo nakala  za  hukumu za miaka  hiyo zipo  kwenye  jengo hilo .
 
Huku  mbunge  wa Kalenga Jackson  Kiswaga  akiomba serikali  kuharakisha  ujenzi wa  mahakama kwa  wananchi  wa  kata ya  Ifunda kutokana na   idadi  kubwa ya  watu kwenye mji wa Ifunda na  Joghorafia ya  kutoka  Ifunda  kwenda Kiponzero .
Wananchi  wa  kijiji  cha Kiponzero  wakitoa  zawadi ya  kuku kwa naibu  waziri wa  katiba ya  sheria Mhe  Pinda 

Mheshimiwa  naibu  waziri wa  katiba ya  Sheria Geofrey  Pinda  akizungunza na wananchi wa Kiponzero 


Ukaguzi  wa   jengo lilokuwa  likitumika kama mahakama ya Mwanzo tarafa ya  Kiponzero 

Nyaraka  za  mahakama ya Mwanzo  Kiponzero zikiwa  zimeachwa  kwenye jengo la awali 

Msasfara  wa  naibu waziri wa  katiba ya  sheria   ukitembelea  iliyokuwa  mahakama ya mwanzo Kiponzero 





Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI