Header Ads Widget

MUME ATUHUMIWA KUUA MKE KISA WIVU WA MAPENZI


MWILI  wa  mwanamke mkazi  wa  kijiji  cha  Mfyome  wilaya ya  Iringa  Salome Kisayo (43)  umekutwa  porini huku  shingoni  kukiwa na alama  za  kucha na nguo yake ya  ndani  ikiwa kando ya  mwili   huo pamoja na kamba  za  miti ya asili  huku mume wake akituhumiwa  kuhusika na mauwaji hayo .


Akithibitisha  kutokea kwa  tukio   hilo  mwenyekiti  wa  serikali ya  kijiji  cha Mfyome  Richard Alyoce  alisema  kuwa  tukio hilo  lilitokea  juzi majira ya saa  3 asubuhi  baada ya  kijana  mmoja kijijini hapo kuona mwili  huo  wakati  akiwa katika harakati za kusafisha  shamba.

''Majira ya  saa 3  asubuhi nikiwa nyumbani kwangu alikuja kijana akaniambia kuna eneo fulani nilikuwa nafanya usafi wa shamba nimemuona mtu jinsia ya kike kama kalala chini, nikamuuliza unahisi atakuwa amekufa akasema ndio nahisi ameshafariki, nikamuita mwenyekiti wa kitongoji husika maana ndio eneo lake, tukaambatana mpaka eneo la tukio na tukamkuta aliyelala pale ni mwananchi aitwaye Salome Kisayo(43) huku pembeni kukiwa na kamba pamoja na nguo zake za ndani huku maeneo ya shingo kukiwa na kucha pamoja na alama za kukabwa'' alisema Richard

Mwenyekiti huyo  alisema  kufuatia tukio hilo  walilazimika kutoa  taarifa polisi  ambao   walipofika kuchukua mwili mpaka hospitali ya mkoa kwa ajili ya uchunguzi zaidi na baada ya hapo walikabidhiwa kwa ajili ya kwenda kuzika.

Hata   hivyo alisema mume wa marehemu aitwaye Belatus Kindole(60)  alitoweka walipokuwa mochwari ambapo mpaka sasa hajulikani alipo na simu zake hazipatikani.

''Huyu mume kwanza kabla ya mimi kupata hizi taarifa alikuja kwangu juzi jumapili  majira ya  saa 9  alasiri kuwa anamtafuta mkewe Salome  na alikuwa na barua ya kitongoji na mimi nikamuandikia barua nyingine ili aweze kwenda vijiji vingine na polisi kutoa taarifa, lakini mpaka inafika hiyo saa tatu asubuhi siku  ya Jumanne niliyopata taarifa kuja kushuhudia hili tukio nilimpigia simu baada ya kuona ni mke wake yule aliyekuwa anamtafuta, lakini ilimchukua kama  saa  hivi hivi kufika hapa  eneo la  tukio tukawa tupo wote mpaka tunaenda mochwari pamoja lakini kufika kule alikaa kidogo na akaondoka , tulipojaribu kumpigia simu zake zilikuwa hazipatikani mpaka muda huu tunaozika hayupo na hatujui yupo wapi'' alisema Mwenyekiti

Alisema  kabla ya tukio hilo la  mauwaji  marehemu  mara kwa mara  walikuwa  wanaishi  kwa  ugomvi na hata siku  mbili kabla ya tukio hilo  walikuwa wamefarakana  na mwanamke  alikimbilia kwa mama yake mzazi .


Mwanaume  huyo  alikwenda kumfuata mkewe kwa mzazi wake  kwa  kumuazima  ili kwenda naye   bustanini  ila ajabu mchana  alirudi  kijijini kudai anamtafuta mkewe  hajarejea  nyumbani  jambo  ambalo lilishangaza  wengi kwa hajawahi kumtafuta mke  mchana kama  huo .

" Kama  viongozi wa  kijiji  tulichobaini   mhusika  wa mauwaji hayo ni mume wake mwenyewe  maana hata kwa ndugu  yake waliooa pamoja  nyumba moja  alidai   siku ya tukio  alifika nyumbani kwake na  kumweleza kuwa amemuua mke wake shambani chanzo ni  wivu wa kimapenzi "


kwa upande wake Diwani wa kata ya Kihwele Felix Waya alisema kuwa hilo ni tukio la kwanza kutokea katika eneo hilo na limewashangaza sana na amewataka wananchi kutoa taarifa kwa uongozi kama kuna jambo lolote linawakwaza hata kama ndani ya ndoa na sio kujichukulia sheria mkononi. 



Kwa  upande  wake dada  wa marehemu Matrida Kisayo  alisema  kuwa  shemeji yake  mara kwa mara alikuwa na ugomvi na mdogo wake na  kuwa  kufuatia mauwaji hayo shemeji mtu  ametoweka  na kuwa  marehemu ameacha  watoto  sita.


Kamanda  wa polisi wa mkoa wa Iringa Juma Bwire alipotafutwa kuzungumzia tukio  hilo  alisema yupo  nje ya  ofisi  kikazi na kuwa kesho   atatoa  taarifa  kamili.





























Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI