Header Ads Widget

KWA MARA YA KWANZA WAKULIMA MBEYA WAPIGA KURA KUCHAGUA MBEGU BORA



NA JACOB SONYO, KYELA -MBEYA


Wakulima wa zao la mpunga wa  skimu ya umwagiliaji kijiji Cha Ngana Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya wameshiriki zoezi la kupiga Kura ili kuchagua mbegu Bora ya zao hilo.



Wakizungumza na Kituo hiki baadhi ya wakulima hao wamesema licha ya kuwepo kwa wingi wa mbegu ya zao hilo lakini bado kumekua na chagomoto hasa katika soko kutokana na kukosa sifa za ziada .



Andrew Mwakipeta ni mmoja wa wakulima wa zao hilo anasema wataalam wamekua wakiwaletea mbegu   bila ya kuwashirikisha jambo  ambalo wamekua wakikumbana na changamoto ya soko licha ya kupata mavuno mengi kutokana na mbegu hizo kukosa sifa  ikwemo ladha, kunukia na muonekano mbaya wa mchele



" mbegu zipo nyingi Sana lakin kila mbegu imekua na sifa yake ila inapokuja sokoni inakosa wateja jambo ambalo bado ni changamoto kwetu "amesema Abdalh 




Taasisi ya utafiti wa  Kilimo Nchini (TARI ) Dakawa kushirikiana na shirika la  AATF kutoka nchini Kenya wanaendesha  zoezi la kushirikisha wakulima Katika tafiti za mbegu bora  ya zai Hilo ili watoe maoni yao wanahitaji mbegu yenye sifa ya aina gani itakayoweza kuwainua kiuchumi.



Barnabas Sitta ni  afisa mtafiti wa TARI Dakawa anasema zoezi hilo litakua lenye mafanikio kwani licha ya Taasisi hiyo kuzalisha mbegu za aina tofauti ya zao la mpunga na  zenye sifa Bora lakin bado zimekua na Changamoto ya mapokezi kwa wakulima .




"tumeona tushirikiane na wakulima Katika tafiti za mbegu tunazozalisha Ili kuondoa malalamiko ya wakulima madai ya  kuletewa mbegu ambazo sio rafiki kwao  kutokana na mazingira na hali ya hewa ya eneo husika" Barnabas Sita mtafiti TARI Dakawa



Kwa upande wake afisa mradi shirika la AATF   kutoka nchini Kenya  Millicent Sedi amesema lengo la mradi huo kuwanufaisha wakulima wa zao hilo Ili kujikomboa kiuchumi.



Sedi amesema wakulima wengi wa zao la mpunga Nchini Tanzania wamekua wakizalisha kwa wingi zao Hilo lakini wameshindwa kujikomboa kiuchumi hivyo tafiti hizi zitaleta tija kwao.



" Tunataka kuwabadili wakulima wa mpunga kutoka Kilimo Cha kizamani kulima Kilimo Cha kisasa hasa Katika uchaguzi wa mbegu Bora "amesema Millicent  afisa mradi AATF 



MWISHO

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI