Afisa maendeleo ya jamii wa halmashauri ya mji Kasulu Azizi Nurfus (kulia) akitoa taarifa ya halmashauri katika usajili wa makundi maalum katika mfumo wa manunuzi ya umma (NeST)
Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru Wazo Mwang'onda (Kushoto) akimkabidhi hati Mkurugenzi wa halmashauri ya mji Kasulu Vumilia Simbeye baada ya halmashauri hiyo kuvuka lengo la usajili wa makundi maalum katika mfumo wa NeST
Kiongozi wa mbio za mwenge Wazo Mwang'onda (kushoto) akizungumza na viongozi wa halmashauri ya mji Kasulu mkoani Kigoma na Mamlaka ya udhibiti wa manunuzi ya umma (PPRA) alipotembelea banda la mamlaka hiyo wakati wa mkesha wa mwenge wa uhuru kwenye halmashauri ya mji Kasulu mkoani Kigoma
Na Fadhili Abdallah,Kigoma
Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru 2026, Wazo Mwang’onda
amezitaka halmashauri za mkoa Kigoma kuhakikisha zinasajili na kutoa tenda kwa makundi maalum ili yaweze kushiriki kwenye mchakato wa manunuzi ya umma kwa taasisi za serikali yanayotoka na asilimia 30 ya bajeti zao za ununuzi za taasisi hizo.
Mwang'onda alisema hayo wakati wa mkesha wa mwenge wa uhuru katika halmashauri ya mji wa Kasulu
mkoani Kigoma akieleza utaratibu huo unaongeza wigo wa ajira kwa jamii na kuyapata uwezo makundi hayo kuwa na shughuli za kufanya badala ya kuwa tegemezi
Kiongozi huyo wa mbio za mwenge alizipongeza halmashauri za Mkoa Kigoma kwa kuweza kufikia na kuvuka malengo ya usajili wa makundi maalum na
kusisitiz kuwa halmashauri za mkoa Kigoma lazima zizingatie kwamba tenda ambazo hazizidi shilingi milioni 500 zinanatolewa kwa makundi hayo maalum kwani kwa sasa makundi mengi yaliyosajiliwa yameonyesha uwezo wa kutekeleza mpango huo.
Awali Meneja wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) Kanda ya Kati na Magharibi, Mhandisi Suma Atupele akitoa taarifa kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, Wazo Mwang’onda alisema kuwa hadi kufikia Septemba saba mwaka huu
Mkoa Kigoma umefanikiwa kusajili Makundi maalum 1359 kwenye Mfumo wa manunuzi ya umma (NeST).
Atupele alisema kuwa pamoja na kupata usajili kwa makundi hayo pia halmashauri za mkoa huo zimetoa zabuni zenye thamani ya Zaidi ya shilingi milioni 500 kwa makundi hayo yanajumuisha vijana, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu na kwamba idadi hiyo imevuka lengo la mamlaka hiyo la kusajili makundi maalum 1200 mkoani Kigoma.
Kwa upande wake Afisa maendeleo ya jamii wa halmashauri ya mji wa Kasulu, Azizi Nurfus alisema kuwa jumla ya makundi maalum 165 yamesajiliwa katika halmashauri hiyo kwenye mfumo wa ununuzi wa kielektroniki (NeST) ambapo kuanzia mwaka 22024/2025 makundi maalum matatu yalipata tenda kwenye halmashauri hiyo zenye thamani ya shilingi milioni 108 kwenye halmashauri hiyo, vikundi viwili vilipata tenda nje ya halmashauri hiyo yenye thamani ya shilingi milioni 253.6 na kikundi kimoja kimepata tenda mbili zenye thamani ya shilingi milioni 74 nje ya mkoa Kigoma.
BONYEZA LINK HII KISHA PIGA KURA ZOTE NNE BAADA YA KUFUNGUA NENDA SEHEMU
BONYEZA LINK HII KUPIGA KURA ZOTE NNE
IMEANDIKWA PIGA KURA KISHA BONYEZA SEHEMU IMEANDIKWA NDIO
MATUKIO DAIMA MEDIA IMETEULIWA KUWANIA TUZO ZA SKA2026 TUNAOMBA KURA YAKO WAWEZA KUPIGA KURA KIRAHISI KULIKO KUPITIA LINK HII










0 Comments