Header Ads Widget

PAPA LEO XIV KUFANYA SAFARI ZA KITUME BARANI AFRIKA, UHISPANIA NA MONACO


 

Papa Leo XIV atafanya safari ya Kitume ya siku kumi kwenda Afrika na nyingine mbili barani Ulaya, Vatican ilitangaza Jumatano.

Ziara ya kwanza itakuwa safari ya siku moja mwishoni mwa Machi hadi Monaco, ikifuatiwa na Safari ya Afrika mwezi Aprili 13-23, na hatimaye Safari ya siku sita kwenda Uhispania na katika visiwa vya Uhispania mnamo mwezi Juni.

Barani Afrika, Papa Leo atazuru Algeria, Angola, Equatorial Guinea na Cameroon.

Zaidi ya Papa Leo italenga amani.

Papa Leo atakwenda katika eneo la wakaazi wanaozungumza Kiingereza kaskazini mwa Cameroon, ambapo kwa miaka kumi kumekuwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe vyenye kuhusisha vikosi vya kawaida vya kijeshi na waasi wanaotaka kujitenga.

Hatua ya mwisho ya Safari hii ya Afrika itakuwa Guinea ya Ikweta, nchi pekee ya Kiafrika inayozungumza Kihispania.

Ziara hii ya Papa inakaribia ile ya Papa Mtakatifu Yohane Paulo II mwaka 1985, alipotembelea nchi saba kwa siku 11.

Kupitia safari hizi tatu za Kitume, Papa Leo atapata fursa ya kukutana na aina na hali mbalimbali za nchi.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI