Mamlaka ya Japan inasema imekamata meli ya wavuvi ya Uchina iliyojaribu kukimbia ilipoamriwa kusimama kwa ukaguzi, katika hatua ambayo inaweza kuzidisha mvutano na Beijing.
Boti hiyo ilikuwa katika eneo la kipekee la kiuchumi la Japan karibu na Mkoa wa Nagasaki kusini-magharibi wakati iliponaswa na nahodha wake kukamatwa siku ya Alhamisi,
Kulingana na wakala wa uvuvi nchini humo. "Nahodha wa meli hiyo aliamriwa kusimama ili kukaguliwa na mkaguzi wa uvuvi, lakini meli ilishindwa kutekeleza agizo hilo na kukimbia," wakala wa uvuvi ulisema.
Ukamataji huo ni mara ya kwanza tangu 2022 kwa shirika hilo kukamata mashua ya uvuvi ya Uchina.
China bado haijajibu kauli ya Japan.





0 Comments