Header Ads Widget

NCAA YAZIDI KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII KUPITIA ROMBO MARATHON

Na,Jusline Marco;Kilimanjaro.

Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imeshiriki katika tamasha la mbili za Rombo lililofanyika leo Desemba 23, 2025,  Rombo Mkoani Kilimanjaro na kuvutia wageni kutoka maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya nchi. 

Mbio hizo zimejumuisha pia watumishi wa Mamlaka hiyo ambao wameshiriki mbio za umbali tofauti hali ambayo inadhihirisha jitihada za NCAA katika kuunga mkono sekta ya michezo,  kutangaza vivutio vya utalii kupitia utalii wa michezo, kujenga uhusiano na wadau kupitia matukio ya kijamii ya kitaifa na kimataifa.


Baadhi ya wananchi waliohudhuria mbio hizo  walipata fursa ya kutembelea banda la Ngorongoro lililowekwa mahsusi kwa ajili ya kutoa elimu kwa washiriki na wananchi kwa ujumla kuhusu shughuli za Uhifadhi na utalii pamoja na mchango wa hifadhi ya Ngorongoro katika kulinda urithi wa asili na wa kitamaduni


.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI