Header Ads Widget

ASKOFU CHILONGANI ATOA WITO WA MAOMBI KUOMBEA AMANI YA TAIFA

 

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba akiwa kwenye Ziara yake ya Kikazi Mkoani Arusha, amesisitiza umuhimu wa kulinda amani kwa maendeleo na ustawi wa Watanzania, akiwataka wananchi kuamka na kuwakataa wale wote wanaowachonganisha kwa maslahi yao binafsi.

Akieleza kuwafahamu baadhi ya Watanzania wanaolipwa fedha ili kuwagombanisha na kuwataka kuingia barabarani kufanya vurugu, Mhe. Nchemba ameeleza kuwa wanaohamasisha vurugu nchini wamekuwa na visingizio kadhaa vya kuwahadaa wananchi huku lengo lao likiwa ni kuwagombanisha watanzania ili kutaka kuzifaidi rasilimali za nchi.

"Zimetokea vurugu, kwa aina  ya vurugu zilivyotokea, kwanini hatushtuki? Wanatumia visingizio vingine lakini hapa kuna mchezo. Zimetolewa fedha wakapewa vijana na wale Vijana wakaandaa Vijana wenzao na kuwataka kufanya vurugu. Leo tujiulize wale wanaotoa hizo fedha watazirudishaje? Na kama ni maandamano, Kiongozi wake alikuwa nani? Waliandamana kutoka wapi kwenda wapi? Ajenda yao ilikuwa ipi? Tunachonganishwa mno, kuna jambo watu wanatafuta. Amkeni Watanzania." Amesema Waziri Mkuu.

Mhe. Mwigulu akizungumza katika Mkutano wake wa hadhara kwenye Viwanja vya Magufuli, Leganga, Usa River, Wilayani Arumeru, amesisitiza kuwa ikiwa Tanzania itapoteza amani na utulivu wake, jamii na serikali itashindwa kukabiliana na umaskini, gharama kubwa za maisha na kukabiliana na tatizo la ajira kwa Vijana, akiwataka Watanzania kutorubuniwa na kuingia kwenye Vitendo vya Uvunjifu wa amani.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI