Header Ads Widget

YALIYOTOKEA HAYAKUWA MAANDAMANO, ZILIKUWA FUJO NA GHASIA DHIDI YA USTAWI WA TANZANIA



Oktoba 29, 2025 nchi yetu ya Tanzania ilishiriki uchaguzi Mkuu wa kuwachagua Diwani, Mbunge na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ndani ya saa 72 Tanzania ikampata Rais, Madiwani na Wabunge ambapo Dkt. Samia Suluhu Hassan tayari ameapishwa Jana Jumatatu Novemba 03, 2025 kuwa Rais wa awamu ya sita akiwashinda wenzake kutoka Vyama 17 vilivyosimamisha wagombea wa nafasi ya Urais.



Oktoba 29, 2025 nchi yetu ya Tanzania ilishiriki uchaguzi Mkuu wa kuwachagua Diwani, Mbunge na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ndani ya saa 72 Tanzania ikampata Rais, Madiwani na Wabunge ambapo Dkt. Samia Suluhu Hassan tayari ameapishwa Jana Jumatatu Novemba 03, 2025 kuwa Rais wa awamu ya sita akiwashinda wenzake kutoka Vyama 17 vilivyosimamisha wagombea wa nafasi ya Urais.


Wakati wa kula Kiapo, Dkt. Samia kama ilivyokuwa wakati akikabidhiwa hati ya ushindi kutoka kwa Tume huru ya Taifa ya uchaguzi, amerejea tena msisitizo wake wa kuwataka Watanzania kutofanya mzaha dhidi ya amani ya Tanzania, akionya kuhusu vurugu zilizotokea katika baadhi ya maeneo nchini hususani katika Miji ya Dar Es Salaam, Mwanza, Arusha na Songwe - Wengi wakimuunga mkono na kuziita ghasia na fujo na si maandamano kama ambavyo baadhi ya wengi wamekuwa wakieleza mitandaoni.


Uhalali wa fujo na ghasia unakuja pia kufuatia kauli ya Jeshi la Polisi na marejeo yaliyofanywa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliyeeleza kuwa taarifa za kiitelejensia zimebainisha kuwa wengi wa waliokuwa wanaongoza ghasia na fujo hizo zilizoambatana na mashambulizi ya kuchoma na kuharibu mali si raia wa Tanzania sambamba na kile ambacho tumekiona Mitandaoni, waliokuwa wakihamasisha ghasia hizo wakiwa pia si wakazi wa Tanzania na wengine ni wale walioukana Utanzania wao na wakiwa na historia za kufaidika pale panapotokea sintofahamu na migawanyiko miongoni mwa Watanzania.


Miongoni mwa wageni wahudhuriaji waliopata fursa ya kutoa salamu zao, amekuwa ni Rais wa Zambia Mhe. Hikainde Hichilema. Katika salamu zake kando ya kuonya Watanzania kutoujaribu upande wa pili wa amani na vile ilivyo ngumu kurejea katika Amani ikiwa itapotezwa, ameshauri wanaohisi kuonewa kutokuwa na chaguo la kuingia barabarani kufanya vurugu na ghasia na badala yake wawe na chaguo sahihi na la kufaa la mazungumzo katika kuondoa na kutatua changamoto zilizopo, akirejea historia ya Taifa lake, kutotendewa haki kwa Chama chake katika chaguzi mbalimbali na namna ambavyo chama chake kiliheshimu, kusimamia na kutetea amani ya Zambia, katikati ya changamoto na vikwazo vilivyokuwepo.


"Sishauri na sitakuwa mshauri wa wananchi na wanasiasa wenzangu kutaka watu waingie barabarani kufanya fujo kama ilivyotokea juzi, hakuna faida ya kufanya hivyo na hakuna namna ambavyo mtafanikiwa kupata haki kwa njia ya fujo na ghasia." Amesisitiza Rais Hichilema wa Zambia.


Ili kudhihirisha kuwa hayakuwa maandamano bali fujo na Ghasia, Mchambuzi Michael Msubya anasema maandamano ni lazima yawe na malengo, yafanyike kwa kuzingatia sheria na yadhamirie kuleta ama kutoa ujumbe fulani ikiwa tu yatakuwa halali kisheria na yenye kuungwa mkono na umma, akionesha kushangazwa na kile kilichofanyika Oktoba 29, 2025.


" Haiwezekani mtake mabadiliko kupitia vurugu na machafuko, haiwezekani mseme mnataka mabadiliko ya mifumo ya uchaguzi au kutuma ujumbe wa kuonewa halafu mnaenda kuchoma vituo vya mafuta vya watu, mnaiba mali za watu madukani na kule Mwanza tumeona wanaenda kuiba mpaka bia kwenye bar za watu, zile zilikuwa vurugu na zinapaswa kupingwa na kila mtu mpenda amani na maendeleo." Ameongeza kusema Bw. Msubya.


Tayari Dkt. Samia kamati za ulinzi na usalama kwenye Mikoa yote ya Tanzania bara zimetekeleza maagizo ya Rais Samia aliyoyatoa hapo jana ya kuhakikisha wanaimarisha ulinzi na shughuli za kijamii na kiuchumi zinarejea katika hali yake ambapo kwa Mikoa mbalimbali nchini Ikiwemo Arusha na Dar Es Salaam, kumeshuhudiwa biashara na masoko ya bidhaa mbalimbali yakifunguliwa pamoja na huduma ya usafiri na usafirishaji ikirejea kama ilivyokuwa awali.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI