Header Ads Widget

WATANZANIA WAHAMASISHWA KUFUATA TARATIBU SAHIHI KUDAI HAKI ZAO

 

Wito umetolewa kwa watanzania wa kutii sheria, kuisikiliza serikali na kutafuta haki kwa namna na taratibu zinazoruhusiwa kisheria badala ya kuratibu na kufanya ghasia, uharibifu na vurugu kama sehemu ya kushinikiza serikali kutekeleza matakwa mbalimbali.

Asraji Likwati, Mwenyekiti wa wasafirishaji abiria kwa njia ya Pikipiki Kimara Mkoani Dar Es Salaam ametoa wito huo leo Novemba 08, 2025 wakati akizungumzia athari za ghasia zilizotokea Jumatano ya Oktoba 28, 2025 siku ya uchaguzi Mkuu wa Tanzania, akiwakosoa baadhi ya vijana ambao walifanya ghasia hizo na kuiba na kuharibu mali na vitega uchumi vya wananchi wa hali ya chini wasiokuwa na nafasi yoyote kisiasa na wasiohusika na kile kilichokuwa kikilalamikiwa na makundi hayo.

"Nitoa wito tu kwamba tuisikilize serikali, haki tuitafute kwa taratibu sahihi kwani ni wengi waliovunjiwa na kuibiwa mfano unaenda kumuibia mangi ambaye hana hata ushawishi na masuala ya kisiasa. Juzi hapa tumelalamika kuhusu mwendokasi serikali ikatusikia na kuleta mabasi mapya, leo wanayachoma moto, kiukweli hii haikubaliki." Amesisitiza Bwana Likwati.

Ameeleza athari nyingine kuwa ni pamoja na kudorora kwa mzunguko wa fedha, kuathirika kwa biashara kati ya Tanzania na nchi jirani zenye kuitegemea bandari ya Dar Es Salaam pamoja na kutikisika kwa sifa ya Tanzania kimataifa ya kuwa Taifa lenye amani, uhuru na mshikamano kwa watu wake.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI