Header Ads Widget

WANANCHI WAHIMIZA UVUMILIVU, MCHAKATO WA MARIDHIANO YA KITAIFA


Kama ilivyoahidiwa na Rais wa Tanzania kwamba moja ya ahadi zake ni pamoja na kutafuta maridhiano ya Kitaifa na kuanzisha mchakato wa Katiba mpya ili kulileta Taifa pamoja na kushughulikia changamoto za wadau mbalimbali, wananchi wa Mkoa wa Dar Es Salaam wamewashauri makundi mbalimbali ya kijamii kuacha mihemko na kuisikiliza serikali, huku serikali pia ikitakiwa kuusikiliza upande wa wananchi kujua kile wanachokitaka.

Kauli za wananchi zinakuja siku chache pia mara baada ya Makamu wa Rais Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi kusisitiza dhamira hiyo ya Rais Samia kuhusu maridhiano ya Kitaifa ili kusikiliza wananchi na kuendelea kuifanya Tanzania kuwa yenye amani na utulivu.

"Ni dhamira ya Rais Samia Suluhu Hassan kuhakikisha tunaanzisha mazungumzo ya maridhiano ili kuhakikisha hata hao wachache wanapata nafasi ya kusikilizwa ili kuwa na taifa lenye amani na umoja na kuendelea kuwa mfano wa utulivu katika Afrika na dunia.”Alisema Dkt. Nchimbi kwenye Mkutano wa Kimataifa uliofanyika siku mbili zilizopita.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wananchi wanaoishi Chanika, Jijini Dar Es salaam wamesisitiza umuhimu wa maridhiano hayo ili kujenga jamii yenye amani na ustawi, wakirejea athari kubwa zilizotokea wakati wa ghasia na vurugu za Oktova 29, 2025.

Wamelaani pia utafutaji wa haki kwa kuhamasisha na kutenda vitendo vyenye kuhatarisha amani ya Tanzania, wito zaidi ukitolewa kwa vijana kuachana na mihemko na ushawishi wa kufanya vurugu na badala yake kupendelea zaidi njia ya mazungumzo na masikilizano katika kushughulikia changamoto zinazowakabili katika maeneo mbalimbali.



 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI