Header Ads Widget

VIJANA TUSISHAWISHIKE KUVUNJA AMANI- MNENGA


Mjasiriamali wa kuosha Magari Jijini Dar Es Salaam Bw. Salum Salum Mnenga ametoa rai kwa Vijana kuwa mstari wa mbele katika kulinda na kuitetea amani ya Tanzania, akisema kukosekana kwa amani kuna gharama kubwa zaidi na wengi ya waathirika wamekuwa wananchi wa kipato cha chini.

Mnenga ametoa kauli hiyo kufuatia vurugu, uharibifu na wizi uliotokea katika maeneo mbalimbali ya Tanzania siku ya uchaguzi Mkuu wa Tanzania Oktoba 29, 2025, akisema vurugu hizo ziliwaathiri zaidi katika uchumi kutokana na kushindwa kuendelea na shughuli zao kwa takribani siku tano mpaka ilipotoka kauli ya Rais Samia Suluhu Hassan kwamba Watanzania waendelee na shughuli zao za kiuchumi na kijamii kama ilivyokuwa hapo awali.

Bw. Mnenga pia amewasihi Vijana kutoshawishika kufanya maandamano ama kujihusisha na matukio ya uvunjifu wa amani, akisisitiza umuhimu wa kuwa na sababu za msingi na kuzingatia sheria na taratibu za nchi kabla ya kufanya jambo lolote lile.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI