Header Ads Widget

WALIOFANYA VURUGU ZA OKTOBA 29, WENGI WALIFUATA MIKUMBO- ABDALLAH

 

Vijana wametakiwa kujiepusha na mikumbo na kufuata yale yanayosemwa katika Mitandao ya Kijamii yakiwa yanahatarisha amani, usalama na Umoja wa Watanzania kwani mambo hayo yana athari hasi zaidi kuliko matarajio chanya waliyonayo Vijana.

Wito huo umetolewa na Hamad Abdallah, Mkazi wa Chanika Jijini Dar Es Salaam kufuatia vurugu na matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea siku ya ya uchaguzi Mkuu na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, akisema jambo lile lilikuwa gumu na lisililokubalika.

Amewasihi Vijana kuachana na mikumbo hiyo, akisema ana uhakika kuwa wengi wa Vijana walioshiriki katika matukio yale ya uhalifu hawakuwa wakijua chanzo na asili ya matukio yale kutokana na wengi wao kuwa wamerubuniwa kupitia kwenye Mitandao ya Kijamii.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI