Header Ads Widget

RC MAKALLA AKUTANA NA VIONGOZI WA DINI ARUSHA, WAFANYA DUA MAALUM KUOMBEA AMANI


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla  amekutana na Viongozi wa dini na wa kimila kutoka Mkoa wa Arusha, akitoa Rai kwa Viongozi hao kuendelea kuhubiri amani kwa waumini na wafuasi wao pamoja na kuiombea nchi ya Tanzania.

CPA Makalla kando ya kujadiliana masuala mbalimbali na Viongozi hao wa dini katika ujenzi wa jamii yenye amani, upendo na mshikamano, alishiriki sala na dua  maalumu iliyoongozwa na Viongozi wa dini na madhehebu mbalimbali akiwemo Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Arusha Sheikh Shaaban Bin Juma na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya maridhiano ya amani Tanzania Dkt. Israel Ole Maasa.

Rc Makalla amesisitiza umuhimu wa Viongozi hao pia kuendelea kuhubiri kuhusu amani na kushirikiana na waumini wao kuliombea Taifa la Tanzania, Viongozi hao wa dini wakiahidi pia kushirikiana na serikali katika kuhakikisha jamii inakuwa na amani na mazingira tulivu.

"Muhimu kuhubiri kuwa hakuna nchi nyingine zaidi ya Tanzania na ili tusonge mbele katika maendeleo ni muhimu kuendelea kuwa na amani na utulivu kwahiyo kila mmoja wetu arejeshe matumaini na maombi hayo kwamba Watanzania tunahitaji amani hivyo sala na maombi yetu kwa Mwenyenzi Mungu ni amani na sisi serikali tutaendelea kupokea ushauri wenu na kuufanyia kazi." Amesisitiza Mhe. Makalla.

Viongozi hao wa dini katika maombi yao, wameombea amani ya Tanzania na kuwaombea Viongozi wakuu wa Tanzania wakiongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na wasaidizi wao wa ngazi mbalimbali akiwemo Mhe. Makalla wakimuomba Mwenyenzi Mungu awape baraka, nguvu na utashi zaidi katika kuwatumikia watanzania na kuhakikisha Tanzania inabaki salama.



 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI