Header Ads Widget

RAIS DKT SAMIA AUNDA TUME KUCHUNGUZA VURUGU ZA UCHAGUZI OKTOBA 29...

RAIS Dkt Samia Suluhu Hassan ameunda Tume Huru ya Uchunguzi kuhusu matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025. Mwenyekiti wa tume hiyo ni Jaji Mkuu Mstaafu Mohamed Chande Othman.


Rais Samia amesema lengo la kuundwa kwa tume hiyo ni kuhakikisha uwazi na uwajibikaji na kwamba matokeo ya uchunguzi yatasaidia kujenga imani ya wananchi na jumuiya ya kimataifa.


Kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka Ikulu, wajumbe wengine walioteuliwa ni:


Profesa Ibrahim Khamis Juma - Jaji Mkuu Mstaafu wa Mahakama ya Tanzania


Balozi Ombeni Yohana Sefue - Mwanadiplomasia na Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu

Balozi Radhia Msuya - Mwanadiplomasia na Balozi Mstaafu

Luteni Jenerali Paul Meela - Mwanadiplomasia na Balozi Mstaafu

Said Ally Mwema - Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania Mstaafu

Balozi David Kapya - Mwanadiplomasia na Balozi Mstaafu

Dkt. Stergomena Lawrence Tax - Aliyewahi kuwa Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI