Header Ads Widget

DKT MWIGULU AFIKISHA SALAMU ZA RAIS DKT SAMIA KKKT AOMBA KUENDELEA KUOMBEA AMANI TAIFA

 



NA MATUKIO DAIMA MEDIA,DODOMA

WAZIRI  Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. Mwigulu Nchemba amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan anaendelea kuwasisitiza Watanzania kuliombea Taifa ili amani, upendo, ustahimilivu na mshikamano viendelee kudumu.


Waziri Dkt Nchemba amesema hayo  leo, Jumapili Novemba 16, 2025, alipowasilisha salamu za Mheshimiwa Rais kwa waumini na viongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kisasa, mkoani Dodoma.


"Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anawasalimu sana. Yuko pamoja nanyi, na rai yake kwa Watanzania ni kuendelea kufanya maombi kwa ajili ya Taifa letu ili liendelee kuwa tulivu," amesema.


Aidha, Waziri Mkuu amesema ni wajibu wa kila Mtanzania kulinda na kuenzi amani, kwani bila amani taifa haliwezi kutekeleza majukumu yake, ikiwemo kuabudu na kuendesha shughuli mbalimbali za kijamii.


"Pasipo amani hatuwezi kutekeleza majukumu yeyote. Pasipo amani hatuwezi kuendesha ibada. Kwa hiyo ni wajibu wa kila Mtanzania kuiombea nchi yetu. Pakiwa na amani tunaweza kutekeleza matarajio yetu, na hata kutatua yale tunayoyaona kuwa magumu,” amesisitiza


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI