Serikali ya Cameroninasema watu wanne wameuawa wakati wa maandamano ya Jumapili katika mji mkuu wa kiuchumi wa Douala, huku hofu ikiongezeka kuhusu mgogoro wa kisiasa nchini humo.
Katika taarifa, Gavana wa mkoa wa Littoral ambao ni kitovu cha uchumi, amesema waandamanaji walishambulia vituo vya polisi na polisi, kwa nia ya kuvichoma moto na vikosi vya usalama vilizuia majaribio haya.
"Katika mapambano hayo, kwa bahati mbaya watu wanne walipoteza maisha," amesema Gavana Samuel Dieudonné Diboua.
Pia amelaani maandamano hayo ambayo akiyaeleza kuwa ni "vurugu zilizopangwa" ambazo ni shambulio kubwa kwa utulivu wa umma na usalama wa taifa.
Zikiwa zimesalia saa 24 tu kabla ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi, mamia ya waandamanaji na wafuasi wa mgombea wa upinzani Issa Tchiroma Bakary walijitokeza mitaani kote nchini na nje ya nchi kukemea kile wanachosema ni udanganyifu wa uchaguzi.
Tchiroma anadai ushindi katika uchaguzi huo, licha ya onyo kutoka kwa serikali.






0 Comments