Header Ads Widget

TUKISEMA UKWELI WANATUITA MACHAWA- SHEIKH KISHKI

 

Mwenyekiti wa Taasisi ya Al- Hikma Islamic Foundation Sheikh Nurdin Kishki amesema wajibu wa viongozi wa dini kote nchini ni kusimamia Amani na mshikamano wa jamii pamoja na kuonya wananchi wasikubali kutumika kwa maslahi binafsi ya watu wanaotaka kuvuruga mshikamano na amani ya Tanzania.

Sheikh Kishki ameyasema haya Leo Jumatatu Oktoba 27, 2025 kwenye kongamano la viongozi wa dini na madhehebu mbalimbali lililofanyika jijini Dar es Salaam, Ajenda kuu ikiwa ni kuilinda na kuitunza amani ya nchi kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Jumatano ya Oktoba 29, 2025.

Kishki amezungumzia pia tabia iliyozuka nchini kwa baadhi ya watu wanaowakebehi na kuwasema Viongozi wanaosema mema ya nchi na kuelekeza kuhusu amani na mshikamano wa Watanzania kwa madai kuwa wanafanya hivyo kutokana na kuwa wanalipwa fedha na Mamlaka.

"Siku hizi ukisimama kulitetea Taifa lako unaambiwa chawa umepewa bahasha na mimi nauliza ninyi mliosimama mstari wa mbele kutaka kutoboa jahazi la MV Tanzania, kutaka kutoboa Taifa hili la Tanzania, Mnapewa bahasha na nani.? Kuna wema na waovu kwenye jamii na Mtume Muhammad anasisitiza kushika na kukamata mikono ya wapumbavu ikiwemo wale wanaowaza nia ovu ya kuidhuru amani ya Tanzania." Amesisitiza Sheikh Kishki.

Kongamano hilo linafanyika wakati huu ambapo zimebaki siku mbili kabla ya uchaguzi Mkuu wa Tanzania hapo Oktoba 29, 2025, ambapo amani imeendelea kuhubiriwa katika makongamano mbalimbali ya kidini na ya kijamii, wakisisitiza kuwa amani ndiyo msingi wa maendeleo na mshikamano unaoshuhudiwa nchini, huku pia wananchi wakihimizwa kujitenga na wote wenye nia ovu kuelekea siku ya uchaguzi Mkuu.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI