Header Ads Widget

NITAKUFA NIKITABASAMU HESHIMA NILIYOWAJENGEA KIGOMA : ZITTO KABWE


 Mgombea ubunge jimbo la.    Kigoma Mjini kwa  Cjama Cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Mwanga Community Centre Mjini Kigoma

Na Fadhili Abdallah,Kigoma

Mgombea ubunge wa jimbo la Kigoma Zitto Kabwe amesema kuwa miaka 15 ambayo amekuwa mbunge katika majimbo mawili ya mkoa Kigoma amejenga heshima kwa wananchi wa mkoa huo ambapo sasa wanatembea na kuona ufahari kutangaza wanatoka Kigoma.

Zitto amesema hayo akihutubia mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika viwanja vya Mwanga Community Centre Mjini Kigoma na kusema kuwa amejenga heshima na utu  kwa  watu wa mkoa Kigoma na kujiona kuwa sasa siyo raia daraja la pili.

Mgombea Ubunge jimbo la Kigoma Mjini ACT Wazalendo Zitto Kabwe (katikati mwenye kofia) na viongozi wa chama hicho wakitembea kwa miguu kuelekea viwanja  vya Mwanga Community Centre ambapo Mgombea ubunge huyo  alihutubia wananchi

Mgombea huyo akisema juwa pamoja na kujenga kujiamini na kuwafanya kuwa watu wanaojenga hoja pia kwa maisha yake ya siasa amepigania changamoto ya watu wa mkoa huo kuonekana siyo raia akitaka uwepo wa usawa katika jambo hilo kama inavyofanywa mikoa mingine ambayo inapakana na nchi jirani.


" Hata sasa nikifuata amrita ya Mungu (kufa) nitakwenda nikitabasamu kutokana na kazi kubwa niliyofanya kuwapigania wananchi wa mkoa Kigoma na sitaacha hadi uhai wa maisha yake, hivyo nichagueni niendelee kupigania maendeleo ya maisha yenu," Alisema Zitto Kabwe.

Akieleza miaka mitano aliyokuwa mbunge jimbo la Kigoma Mjini (2015 - 2020) alisema kuwa kwa kusaidiana na idadi kubwa ya madiwani na meya waliyokuwa nayo walifanya kazi kubwa ikiwemo kuimarisha barabara za manispaa ya Kigoma Ujiji, kuimarisha biashara kwa kujenga masoko na kuanzisha miradi ambayo imekuwa na chachu kubwa ya kujenga uchumi wa wananchi wa manispaa hiyo.


Katika hilo alisema kuwa wametengeneza mabango na kusambaza mji mzima kuonyesha ushahidi ili wasionekane waongo hivyo alitaka mwenye hoja anayepinga maneno yake aonyeshe kwa vitendo kwa ushahidi.

Awali Mgombea Mwenza wa Uraisi wa Chama Cha ACT Wazalendo, Fatma Fereji alisema kuwa wananchi wa jimbo la Kigoma Mjini watafanya kosa kubwa na ambalo watalijutia kama hawatamchagua Zitto Kabwe kwani amekuwa mtetezi mkubwa wa mambo yanayogusa maisha yao.

Naye Mwenyekiti wa ngome ya vijana Taifa na Kampeni Meneja wa Mgombea huyo, Abdul Nondo alisema kuwa Zitto amekuwa Mwalim wa siasa, Mlezi wa vijana lakini mpambanaji wa maendeleo ya wananchi wa mkoa Kigoma na aliyofanya ushahidi unaonekana hivyo haina sababu y kutumia nguvu kubwa kulielez hilo wakati kila kitu kinajieleza wazi.



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI