Header Ads Widget

LIWAKA AFUNGA KAMPENI KWA KISHINDO NACHINGWEA

  


Na Hadija Omary 

MGOMBEA Ubunge Jimbo la Nachingwea Mkoani Lindi kupitia chama cha mapinduzi CCM Bwana Fadhiri Liwaka Leo amefunga rasmi kampeni zake za kusaka Kura za Rais, wabunge na Madiwani huku akiahidi kushirikiana na wananchi wa Jimbo hilo Katika shughuli za kimaendeleo ikiwa pamoja na kusimamia ujenzi wa barabara ya  Nachingwea Masasi kwa kiwango cha lami 

Liwaka amefunga kampeni hizo Leo oktoba 27/2025 Katika viwanja vya mauridi katika Kata ya Nachingwea Wilayani humo ikiwa ni saa chache kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika hapo kesho


Liwaka alitaja vipaumbele vyake sita ambavyo ni kutatua tatizo la maji,  barabara , huduma za Afya,  jenzi wa madarasa ambavyo atashirikiana na wananchi wa Jimbo hilo mara baada ya kuchaguliwa kwake na kuapishwa kuwa Mbunge wa Jimbo hilo 

Ikumbukwe kuwa Fadhiri Liwaka nigombea pekee wa Ubunge Katika Jimbo Hilo la Nachingwea 



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI