Header Ads Widget

KUSHAMBULIWA KWA MABASI YA MWENDOKASI TANZANIA: WATATU WAKAMATWA.

 

Watu watatu wamekamatwa nchini Tanzania kufuatia vurugu zilizozuka baada ya watu wasiojulikana kushambulia mabasi yaendayo haraka maarufu kama mwendokasi.

Kulingana na Taarifa iliotumwa kwa vyombo vya habari, watatu hao wanaendelea kuhojiwa na polisi huku chanzo cha matukio hayo kikifuatiliwa na maafisa hao.

Aidha taarifa hiyo imesema kwamba watuhumiwa wengine waliohusika na tukio hilo wanatafutwa.

Picha za video zilizosambaa mitandaoni hapo awali zilionyesha baadhi ya vioo vya mabasi na vituo vikiwa vimevunjwa baada ya kushambuliwa kwa mawe usiku wa kuamkia leo Jijini Dar es Salaam.

Hivi karibuni njia hiyo ya usafiri inayotegemewa na maelfu ya wakaazi wa jiji hilo kubwa zaidi nchini Tanzania imekumbwa na malalamiko ya wananchi kutokana na uhaba wa mabasi ikilinganishwa na idadi ya abiria.

Hata hivyo jumatano asubuhi mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Albert Chalamila alifanya ziara ya kushtukiza katika kituo kikuu cha mabasi ya mwendo kasi na kuwaomba radhi watumiaji wa usafiri huo na kuwataka kuwa na subira wakati serikali ikiendelea na mipango ya kutatua adha wanazozipitia ikiwemo kuongeza idadi ya mabasi.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI