Header Ads Widget

KISABYA WA NRA ATAKA BARAZA DOGO LA MAWAZIRI

 

  Mgombea Urais wa Chama cha NRA akihitimisha kampeni zake katika uwanja wa           Community Centre mjini Kigoma

Na Fadhili Abdallah,Kigoma

MGOMBEA Uraisi wa Chama Cha National Reconstruction Alliance (NRA) Almas Hassan Kisabya amesema kuwa akichaguliwa kuwa Rais wa Tanzania atapunguza ukubwa wa baraza la mawaziri ili kupunguza mzigo wa matumizi kwa serikali. 

Kisabya alisema hayo akihitimisha mikutano yake ya kampeni ya Uraisi alipofanya mkutano kwenye viwanja vya Mwanga Community Centre mjini Kigoma na kubainisha kuwa baraza la sasa la mawaziri linaigharimu serikali kiasi kikubwa cha fedha katika uendeshaji wake.

Alisema kuwa pamoja na kuwa na baraza kubwa la mawaziri sehemu kubwa ya mawaziri waliopo wamekuwa wakifanya mambo kwa kuwaza uchaguzi ujao badala ya kutumia utaalam walionao na nafasi zao katika kuwatumikia watanzania. 


Ameonya kuwa Watanzania wanapaswa kufanya maamuzi sahihi wanaposhiriki kwenye uchaguzi kwa kuchagua mtu ambaye ana nia na dhamira ya dhati ya kuwatumikia watanzania badala ya kuwachagua watu kwa umaarufu wao au uwezo wa kifedha waliona na mambo ambayo yatawagharimu kwa miaka mitano.

Akizungumzia suala la elimu alisema kuwa serikali zilizopita na iliyopo madarakani zimefanya kazi kubwa katika ujenzi wa shule za msingi na sekondari na kwamba kazi kubwa iliyopo ambayo ni changamoto kubwa ni uendeshaji wa shule hizo hasa kuzingatia mambo yanayoweza kuinua taaluma ikiwemo uhaba wa walimu, wanafunzi kukaa chini na ukosefu wa nyumba za walimu.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI