Header Ads Widget

RAIS CHAKWERA AKUBALI KUSHINDWA UCHAGUZI MALAWI

 

Rais Chakwera amekubali kushindwa, na kuliambia taifa la Malawi kuwa anafanya hivyo kwa kuheshimu nia yao ya kutaka mabadiliko ya serikali.

Rais Chakwera akihutubia taifa kabla ya matokeo ya uchaguzi mkuu kutangazwa leo mchana.

Matokeo ya awali yanaonesha mpinzani wake, Rais wa zamani Peter Mutharika ameongoza vyema, akijizolea karibu asilimia 66 ya kura zilizohesabiwa kufikia Jumanne. Chakwera alikuwa amepata 24%.

Katika hotuba yake, Chakwera alitambua matokeo ya kura za awali, jambo ambalo lilionyesha mpinzani wake Peter Mutharika alikuwa ameongoza kwa kiasi kikubwa.

"Ninajua kwamba kwa wengi wenu mliopiga kura, matokeo haya ni taswira ya nia yenu ya pamoja ya kuwa na mabadiliko ya serikali na hivyo ni sawa kukubali kushindwa kutokana na kuheshimu matakwa yenu kama raia," aliwaambia Wamalawi.

Chakwera anasema amempigia simu Mutharika kumpongeza kwa "ushindi wake wa kihistoria".

Alithibitisha kuwa alifika mahakamani jana kujaribu kuzuia matokeo yasitangazwe lakini akasema anakubali uamuzi wa mahakama kwamba tume ya uchaguzi lazima iendelee na kutangaza matokeo.

Chakwera pia alisema: "Wamalawi, kama mko upande wa kushindwa au kushinda, tafadhali muwe na amani."


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI