Header Ads Widget

MKUTANO WA KAMPENI WA MGOMBEA MWENZA WA URAIS CCM DKT NCHIMBI PAWAGA JIMBO LA ISMANI

 Mgombea mwenza wa urais kupitia chama cha mapinduzi (CCM) balozi Dkt Emanuel Nchimbi ameomba wananchi wa Jimbo la Isman kumpa kura za kutosha Mgombea Urais Dkt Samia Suluhu Hassan na katika ubunge kumpa Wiliam Vangimembe Lukuvi na madiwani wa CCM .

Alisema Kazi zolizofanywa na Rais Dkt Samia kwa kushirikiana na mbunge Lukuvi katika jimbo la Isman ni kubwa na ili kazi hizo kuendelea kufanyika wananchi hawanabudi kukichagua chama cha mapinduzi .

Dkt Nchimbi alisema Lukuvi ni mwalimu wake kisiasa na mshauri wake na alimtabiria kuwa atafika mbali na leo anauona utabiri wake.

Hivyo alisema wana CCM hawakukosea kumchagua Lukuvi kuwa mgombea wao Ubunge kwani kazi hiyo anaifahamu na ataendelea kuwatumikia vema .

 Kuhusu maendelea jimbo la Ismani alisema CCM kimejipanga kuimarisha miradi mbalimbali ya maendeleo katika jimbo la Isimani mkoani Iringa ili kukuza uchumi wa jimbo hilo.

Dkt Emmanuel Nchimbi alipokuwa akizungumza na wananchi katika uzinduzi wa kampeni jimbo la Ismani katika kata ya Itunundu leo.

Balozi Nchimbi amesema katika jimbo la Ismani wamejipanga kutekeleza ilani katika sekta ya afya kwa kuboresha Hospitali ya wilaya, ujenzi wa vituo vya afya pamoja na ujenzi wa zahanati.

akizungumzia sekta ya maji Balozi Dkt. Nchimbi amesema wamejipanga kutekeleza ilani ya chama cha mapinduzi kuchimba visima virefu vya maji katika jimbo la isimani ikiwa ni pamoja na kuboresha mabwawa ili kuendeleza sekta ya kilimo na ufugaji.

kuwa katika sekta ya elimu wamejipanga kujenga shule mpya za sekondari, shule za msingi .


Kwa upande wa Lukuvi alipongeza kazi kubwa zilizofanywa na serikali ya wamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia katika jimbo la Ismani kuwa miradi mingi imetekelezwa ambayo ni ukombozi kwa wananchi .

Miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa barabara lami  ya Ruaha- Samora   itagharimu Kiasi cha Tsh billioni 142.5.

Alisema   hivi  sasa  wakandarasi  wa  ujenzi  wa  barabara  hiyo wapo  barabarani na bahati mbaya  wameanzia  mwisho  kuja  mjini lakini  utawaona na kazi inakwenda  vizuri  sana  lakini huu ni mradi wa  kielelezo kwani  huu mradi unaunganisha mkoa mzima  na  hii hifadhi ni kubwa sana Tanzania ni Hifadhi ya  pili  kwa ukumbwa  nchini  na mradi huu wa ujenzi wa barabara  unakwenda na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Nduli na hii ndio  ilikuwa  ndoto yangu  mwaka  1995  nilipokuwa  nikigombea ubunge kila mmoja anajua.

 

Lukuvi  alisema  jambo la pili kubwa kwa jimbo la Isiman kuwa wakati  anaingia ubunge mwaka 1995    shule  ya sekondari  Tangu 1995 sekondari zilikuwa ni  15 zikizojengwa kwa kipindi cha miaka 25 ni 9 na zilizojengwa  kipindi cha awamu ya sita chini ya Dkt Samia zilizojengwa kwa kipindi cha miaka 25 ni 9 na zilizojengwa awamu ya sita inayoongozwa nawe Dr.Samia S.Hassan*


"sisi  leo   tuna sekondari 15 lakini katika miaka  25  tumejenga  shule 6 tumejenga maana yake sisi na wananchi  serikali ilikuwa ndio  ilikuwa inatuunga mkono  leo  miama  minne  yako  mheshimiwa Rais Dkt Samia umejenga  shule sita za serikali bila wananchi kutoa pesa  sasa  hata kwa uwiano wa  hesabu za kawaida  wa miaka 25 na minne utaona  kazi kubwa  uliyofanya"*


 Kuwa   hizo  ni shule  zote   lakini  tumechelewa sana  kupata  'A' Level  kwani kwa kipindi changu chote cha miaka 25  jimbo la  Isman tulikuwa na A level  nne  lakini wewe  hivi  sasa kwa kipindi cha miaka  minne umeongeza  shule za  A level nne kwa  hadi sasa  shule  zipo nane  kati ya hizo nne  zimejengwa kwa kipindi cha miaka 25 na nne kwa  kipindi cha miaka nne ya Dkt  Samia madarakani .


Mheshimiwa   pamoja na hizo  shule lakini leo  jimbo la Isman umeanzisha mapinduzi kwenye  sera ya elimu  tunataka kwenda kwenye  elimu ya kujitegemea lakini deni hilo kwa jimbo la Isman  umeshalipa  kuna chuo  cha  VETA Pawaga  jimbo la  Isman ambacho   vijana masikini wanachangia  kiasi cha Tsh 150,000 tu  wanapata  kitanda  ,chakula na kila kitu  kwa  Tsh 150,000.


Aidha  Lukuvi  alisema  kw upande wa vituo vya afya  katika  miaka  25  yote   jimbo la  Isman halijawahi kujengewa  hata   kimoja sio kwamba  havipo  vilikuwepo  vinne kwa miaka yote  25  ila  Zamani  tulikuwa  tunachukua  Zahanati hivi  na kugeuza kituo cha afya halafu  tunaongeza  wodi mbili  na sisi kati ya  vituo  hivyo  kimoja  alikuja  Marehemu  Makamu  wa Rais Dkt  Omary  akakizindua  lakini ilikuwa Zahanati  kituo  cha faya  hivyo kwa miaka  25  kulikuwa na  Zahanati  nne  zilizopandishwa hadhi na kuwa vituo vya  afya lakini miaka  minne hii ya kwako  vituo vilivyojengwa toka  kwenye msingi vinne  vipo  jimbo la Isman vimeanza kutumika lakini  kipo kimoja  cha Ilolompya  na Mahuninga  pesa  zipo  huko  huko  milioni 800 za  kukamilisha  ujenzi  huo .


Lakini baadae  vituo  vipya   vya Migoli  ,Isman na hospitali ya wilaya na kuletewa  gari  za wagonjwa mwaka jana    kwa  hiyo unaweza kujua kuwa hawa  wananchi wa Isman wanafuraha  kiasi  gani kwa kazi kubwa  walizofanyiwa  na  serikali hii ya  awamu ya sita   kwani  huduma  za afya  bora  zaidi na  madaktari  wapo mfano hapo  Isman leo kuna madaktari kutoka  huku  Duniani walikuja kufanya kambi ya  macho  watu  8000 wamepata  huduma pale kwa sababu kuna mashine ya upasuaji  na hivyo hata wagonjwa kuja  mjini kutibiwa  kwa sasa  hawafiki kabisa .


Pia  alisema  hata  Hospital ya  wilaya   iliyojengwa na serikali  ya  awamu ya sita  ipo   jimbo la  Isiman Pawaga   pia  alisema kuhusu  huduma  ya  maji  wananchi wa tarafa ya Isman toka  nchi  ipate  Uhuru  hawajawahi  kuwa na huduma ya maji ya  bomba  na kwa kipindi chake  chote  cha ubunge amekuwa akibadili kila aina  ya msamiati  kuhusu  kero ya maji  lakini leo  maji   yanatoka  Isman yote tena maji ya  bomba  safi  na  salama  .


" kwa  kuwa  Ismani  hakuna chanzo  cha maji  wewe  uliagiza maji yavutwe  kutoka  Iringa mjini  na mengine kutoka  Kilolo  na  mradi  huo  umetekelezwa maji wananchi  wanapata  tena  vijiji  vyote  kiasi cha Tsh  Bilioni 9 zimetumika  kusogeza  huduma ya  maji na  sasa  mamlaka ya maji  safi na usafi wa mazingira  Iringa (IRUWASA) ambayo ndio inatekeleza mradi huo uimeomba Tsh bilioni 3  ili  kukamilisha kusogeza  huduma  ya maji kwenye  vitongoji  pia  mheshimiwa Rais  haya  ninayoyasema  naomba  sana watu  wa Isman wawe wanakuangalia sana wewe  maana   kila  wakati  wamekuwa wakisema wanakuombea  sasa  leo umekuja  mwenyewe"


Hata  hivyo  Lukuvi  alisema  ukiacha tarafa  mbili ya  Isman ,tarafa mbili  zimebalikiwa sana  maana  zinazungukwa na mto Ruaha  ambao  unamwaga maji yake  bwawa la Mtera  lakini maji hayo yamekuwa hayatumiki  kwa uzalishaji  ila  sasa  baada  ya  kipindi cha miaka minne ya  Dkt  Samia mto  huo umekuwa  mkombozi mkubwa kwa  wananchi wake.



 Kuwa kwa kipindi chake Dkt Samia ameleta pesa kwa ajili ya liomba ujenzi wa mradi mkubwa wa  umwagiliaji Pawaga Unaitwa Mkombozi  wenye Bilioni 59.9   na kama haitoshi ameongeza pesa kiasi cha  Tsh  Bilioni 33.8 kwa ajili ya mradi wa umwagiliaji wa  Magozi  miradi itakayoongeza kipato cha mtu mmoja mmoja na miundo mbinu ya  barabara kwa Pawaga kuwa na sehemu ya lami kidogo ikimpendeza japo haipo kwenye ilani basi kufikiliwa kuwa na wilaya ama Halmashauri yao wenyewe .


Pia  alisema  kwa  wananchi  wa  Ismani kutokana na ukame  wanaomba  kama  inawezekana kupata  mabwawa ya umwagiliaji  ili  yaweze  kutumika  kipindi cha  kiingazi kwa  ajili ya  shughuli za uzalishaji  hivyo  alisema  kwa kuwa kipindi hicho ni cha kampeni za uchaguzi  kwa niaba ya  wananchi wa Isman wanahidi kutiki  kura zote za ndio  kwa mgombea Urais wa CCM Dkt  Samia Suluhu Hassan kura ambazo mgombea mwingine yeyote hajawahi kupata ,Mbunge wa  CCM na  madiwani wote wa CCM  Oktoba 29mwaka huu.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI