Mkuu wa wilaya Kigoma Dk.Rashid Chuachua
Na Fadhili Abdallah,Kigoma
Mkuu wa wilaya Kigoma Dk.Rashid Chuachua amewataka wananchi wa mkoa Kigoma kujitokeza kwa wingi kumpokea na kumuonyesha upendo Rais Samia Suluhu Hassan ambaye atafanya ziara ya siku mbili mkoani Kigoma kuanzia tarehe 13 mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mkuu huyo wa wilaya Kigoma alisema kuwa Rais Samia ataingia mkoani Kigoma Septemba 12 akitokea mkoani Tabora ambapo tarehe 13 Agosti atafanya mikutano katika wilaya za Uvinza, Kasulu na Buhigwe.
Sadiki Kadulo Katibu wa CCM wilaya Kigoma Mjini (kulia) akizungumza katika mkutano na waandishi wa habariDk.Chuachua alisema kuwa tarehe 14 Rais Samia atafanya mkutano mkubwa wa kampeni katika viwanja vya Katosho Manispaa ya Kigoma Ujiji ambapo aliwataka wananchi wote kujitokeza kwa wingi kusikiliza sera, ilani na mambo ambayo serikali imeyafanya lakini pia ataeleza mipango ambayo serikali yake itafanya kwa miaka mitano ijayo.
0 Comments