Header Ads Widget

BARAZA LA USALAMA LA UMOJA WA MATAIFA KUFANYA MKUTANO WA DHARULA KUHUSU DRONI ZA URUSI NCHINI POLAND

 

Kwa ombi la Poland, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa litafanya mkutano wa dharura kujadili ukiukaji wa Urusi wa anga ya Poland, Reuters iliripoti, ikiinukuu Wizara ya Mambo ya Nje ya Poland.

Hatua hiyo ilikuja kujibu oparesheni ya usiku moja ambayo Warsaw, ikisaidiwa na washirika wa NATO, ilitungua ndege kadhaa zisizo na rubani za Urusi ambazo zilikiuka anga yake siku ya Jumatano.

Katika siku ya shambulizi wizara ya ulinzi ya Urusi ilisema haikupanga kushambulia maeneo yoyote nchini Poland, baada ya Warsaw kusema ndege 19 zisizo na rubani za Urusi ziliingia kwenye anga yake wakati wa mashambulizi ya usiku magharibi mwa Ukraine

Aidha wizara ya Mambo ya nje ya Urusi ilisema Poland imekuwa ikieneza "simulizi za uwongo" kuhusu uvamizi wa ndege zisizo na rubani ili "kuzidisha mzozo wa Ukraine". ."Hata hivyo, tuko tayari kufanya mazungumzo na wizara ya ulinzi ya Poland kuhusu suala hilo."

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI