Header Ads Widget

ZELENSKY ASEMA YUKO TAYARI KWA MAZUNGUMZO YA PUTIN HUKU ULAYA IKIFURAHISHWA NA HAKIKISHO LA USALAMA WA TRUMP

 

Rais Volodymyr Zelensky amesema yuko tayari kwa mazungumzo ya Putin huku Ulaya ikifurahishwa na hakikisho la usalama wa Trump.

Zelensky amesema kuwa hakuna tarehe iliyothibitishwa kwa mazungumzo yoyote yajayo kati yake na Putin na kuwa "wamethibitisha tu baada ya mkutano huu wenye tija na rais," kwamba mazungumzo yataendelea kati ya Ukraine na Urusi.

Zelensky alisema "imethibitishwa kwamba wako tayari kwa mkutano wa pande tatu," lakini akaongeza kuwa "ikiwa Urusi ilipendekeza kwa rais wa Marekani mkutano wa kidiplomasia kati ya pande zinazowakilisha nchi mbili, pia tutaona matokeo yake".

"Ukraine haitakuwa kikwazo cha kufikia amani," alisema.

Hayo yanajiri baada ya Trump kumpigia simu Putin wakati wa mkutano wa White House ukiendelea.

"Wakati wa kuhitimisha mikutano hiyo, nilimpigia simu Rais Putin, na kuanza maandalizi ya mkutano katika eneo litakaloamuliwa kati ya marais Putin na Zelenskyy," aliandika.

"Baada ya mkutano huo kufanyika, tutakuwa na mkutano wa pande tatu, ambao utakuwa Marais wawili, pamoja na mimi mwenyewe."

Trump pia alisema dhamana ya usalama kwa Ukraine ilijadiliwa wakati wa mazungumzo ya leo, ambayo alisema "itatolewa na Nchi mbalimbali za Ulaya, kwa uratibu na Marekani".

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI