Header Ads Widget

MAFANIKIO YA TADB YAMPA RAHA RAIS SAMIA


 ……Nyabundege aweka wazi mabilioni yaliyotolewa na Rais Samia miana minne

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

RAIS Samia Suluhu Hassan, ameipongeza Benki ya Maendeleo  ya Kilimo (TADB) kwa kazi nzuri  iliyofanywa na benki hiyo  katika kuleta mageuzi makubwa kwenye Sekta ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi.

Alitoa pongezi hizo jana wakati alipotembelea banda hilo kwenye kilele cha amaonyesho ya wakulima nanenane yaliyofanyika kwenye viwanja vya Nzuguni Dodoma.

Alisema ndani ya muda mfupi TADB imekuwa msaada mkubwa kwa wakulima ambapo waliwapa mikopo iliyowawezesha kulima kisasa na kuongeza tija kwenye kilimo chao.

TADB kama Mdhamini Mkuu wa maonesho ya Nanenane amekuwa kuvutio kikubwa kwa wananchi waliotembelea maonesho hayo kupitia  elimu iliyokuwa inatolewa kwa njia ya madarasa, shuhuda za wanufaika, machapisho pamoja  na maelezo ya moja kwa moja.


TADB,inaendelea kuthibitisha dhamira yake ya kuleta mapinduzi ya kilimo kwa vitendo kupitia elimu ya kifedha, mikopo ya kimkakati, na uwezeshaji wa wakulima wadogo na wa kati. Ameyasema Hayo mbele ya  ya Mhe. Rais.


 Mkurugenzi Mkuu wa TADB,  ameongezea kuwa leo tarehe  TADB inasherehekea kutimiza miaka 10 tangu kuanzishwa kwake na imepata mafanikio makubwa zaidi ya asilimi 80 chini ya   Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan.

Nyabundege akiongea kwa niaba ya wadhamini wengine toka kwenye taasisi za kifedha kuwa TADB utaendelea kuwa mdhamini mkuu kwa miaka mitano mfululuzo


 TADB kwa sasa imeingia kwenye orodha ya mabenki makubwa nchini Tanzania, imeweza kuwafikia wanufaika wengi  zaidi, na kujijengea heshima Kitaifa na Kimataifa.

Zaidi ya wakulima milioni 1.95 wamefikiwa na ndoto zao kupitia TADB, huku zaidi ya TZS trilioni 1.13 zikitolewa tangu 2015 kama mtaji wa mabadiliko kwa kilimo cha Tanzania.

TADB si tu benki ni nguzo ya matumaini, injini ya uzalishaji, na daraja la maendeleo kwa wakulima wa Tanzania.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI