Header Ads Widget

IDADI YA VIFO YAONGEZAKA SANAA BAADA YA MASHAMBULIZI YA ANGA ISRAEL


 Televisheni ya Al Masirah yenye uhusiano na Houthi imeinukuu Wizara ya Afya ya Yemen ikisema kuwa, idadi ya waliofariki kutokana na mashambulizi ya anga ya Israel dhidi ya Sanaa imeongezeka na kufikia sita, huku wengine 86 wakijeruhiwa.

Wizara hiyo imesema, "Raia sita waliuawa na wengine 86 walijeruhiwa kutokana na hujuma ya Wazayuni kwenye kituo cha umeme cha Haziz na kampuni ya mafuta kwenye barabara ya 60." Idadi iliyotangazwa hapo awali ya vifo ilikuwa niwatu wanne waliokufa na majeruhi 67 .

Alisema kuwa "Vikundi vya Ulinzi wa Raia na uokoaji bado vinatafuta na kutambua watu waliopotea."

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alisema kuwa mashambulizi ya anga ya Israel dhidi ya Sanaa yaliharibu ikulu ya rais mjini Sanaa, pamoja na kituo cha umeme cha mji huo. Alisisitiza kuwa kundi linaloungwa mkono na Iran "linalipa gharama kubwa kwa mashambulizi yake dhidi ya Israel."

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alisema kuwa mashambulizi ya anga ya Israel dhidi ya Sanaa yaliharibu ikulu ya rais mjini Sanaa, pamoja na kituo cha umeme cha mji huo. Alisisitiza kuwa kundi linaloungwa mkono na Iran "linalipa gharama kubwa kwa mashambulizi yake dhidi ya Israel."

Wakati huo huo, kanali yenye uhusiano na Houthi ilitangaza kwamba mashambulizi ya anga ya Israel yalilenga mji mkuu wa Yemen, Sanaa, siku ya Jumapili. Imewanukuu wakazi wa mji mkuu huo wakisema kuwa mashambulizi hayo ya anga yalilenga maeneo karibu na kambi ya rais, vituo vya makombora, na vinu vya mafuta na nishati.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI