Zaidi ya Warundi milioni sita wamejitokeza kwa wingi kushiriki duru ya mwisho ya uchaguzi wa viongozi wa taasisi mbalimbali za kitaifa, mchakato ulioanza mwezi Juni.
Jumatatu ya tarehe 25 Agosti, wananchi wanapiga kura kuwachagua viongozi 3,044 wa vijiji na mitaa kutoka maeneo yote ya nchi, ambao watatumikia kwa kipindi cha miaka mitano.
Awamu za awali za uchaguzi zilifanyika mwezi Juni kwa wabunge na madiwani, na Julai kwa wagombea wa vyama vya upinzani.
Katika chaguzi hizo, chama tawala cha CNDD-FDD, ambacho kimeiongoza Burundi kwa zaidi ya miaka 20, kilitangazwa mshindi kwa asilimia 100 ya kura katika nafasi nyingi isipokuwa kwenye nafasi za madiwani wa halmashauri, ambako kilikabiliwa na ushindani mkali na kupoteza kwa chini ya asilimia 2.
Hii ni mara ya kwanza kwa chama hicho kushinda kwa kiwango hicho kikubwa tangu kipate madaraka, licha ya ushindani kutoka kwa zaidi ya vyama 20 vya siasa vilivyoshiriki uchaguzi.
0 Comments